NYUMBANI KITAIFA

Ulimwengu wa habari.

KATIKA BIASHARA

Ulimwengu wa habari.

MATAIFA MENGINE

Ulimwengu wa habari.

KATIKA BURUDANI

Ulimwengu wa habari.

MAAJABU DUNIANI

Ulimwengu wa habari.

Thursday, December 13, 2012

WANABLOG TUJIFUNZE KATIKA HILI


Mahakama ya Katiba Misri

Kutoka Misri
MAHAKAMA moja nchini Misri imempa mwanablogu mmoja kifungo cha miaka mitatu gerezani kwa kukufuru na kudharau dini.

Alber Saber alikamatwa mwezi wa tisa baada ya majirani kumlaumu kwama ndiye aliweka kilinganishi cha mtandao kilichoashiria sinema iliyoidhihaki dini ya Kiisilamu, na iliyosababisha maadamano makali katika ulimwengu wa Kiislamu.
Bwana Saber, ambaye haamini Mungu yeyote na anayetoka familia ya Kikristo ya dhehebu la Coptic, anaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo iwapo atalipa dola 167 kama dhamana.

Kesi hii inazua maswala nyeti kuhusu uhuru wa maoni wakati raia wa Misri wakijiandaa kupiga kura ya maoni kuhusu katiba rasimu.

Wito Kutaka aachiliwe
Wanaharakati wa haki za banadamu wametoa wito kuwa Bwana Saber achiwe huru.

Kumekuwa na kesi kadhaa zinazohusiana kukufuru baadhi ya mambo nchini Misri katika miaka miwili tangu Hosni Mubarak apinduliwe, huku wengi wa washtakiwa ni wa dhehebu la Copts, ambao ni asilimia 10 ya idadi ya watu nchini humo

Ingawaje kumkufuru Mungu limekuwa kosa la jinai kwa miaka mingi, Kifungu 44 cha katiba rasimu kina kifungu maalum kinachopiga marufu kashfa dhidi ya manabii.
Chanzo: BBC

Wednesday, December 12, 2012

PICHA 3 ZA CAKE YA BIRTHDAY YA WOLPER



RAIS DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE AONGOZA WATANZANIA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 51 YA UHURU WA TANZANIA UWANJA WA UHURU


Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dk.Jakaya Kikwete akiwasili katika gari maalum la Kijeshi na Mkuu wa majeshi Jenerali Davis Mwamunyange kwenye uwanja wa uhuru kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 51 Uhuru wa Tanzania Bara 2012 yanayofanyika kila mwaka Desemba 9, Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Mwaka huu ni “Uwajibikaji, Uadilifu na Uzalendo ni nguzo ya Maendeleo ya Taifa letu”
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya Ulinzi na usalaama katika maadhimisho hayo.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya Ulinzi na usalaama katika maadhimisho hayo
Kikosi cha Brass Band cha majeshi ya Ulinzi na usalama kikitumbuiza katika maadhimisho hayo
Viongozi mbalimbali wakiwa katika maadhimisha hayo kutoka kulia ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mama Maria Nyerere, Rais wa Msumbiji Mh. Armando Guebuza,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib Bilal na Mzee Ali Hassan Mwinyi rais Mstaafu wa awamu ya pili
(PICHA NA FULLSHANGWEBLOG.COM)
Rais wa Msumbiji Mh. Armando Guebuza akipokewa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Said Meck Sadik mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa.
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mh. Joseph Kabila akipokewa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Said Meck Sadik mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Uhuru asubuhi hii.
Mama Maria Nyerere akiwasili kwenye uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanzania.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda akiwasili kwenye uwanja wa Uhuru kuhudhuria maadhimisho hayo huku akisindikizwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Said Meck Sadik.
Mzee Ali Hassan Mwinyi akiwasili kwenye uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho hayo.
Vikosi vya Ulinzi na Usalama vikiwa vimejipanga tayari kwa gwaride la utii na heshima mbele ya Amiri jeshi Mkuu na Rais Jamhuri ya muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete.
Makamu wa Rais Dk. Gharib Bilal akisalimiana na Mama Fatma Karume mara baada ya kuwasili uwanjani hapo, katikati ni Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda.
Rais Jakaya Kikwete akipokea gwaride la heshima wakati wa maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanzania Bara yanayofanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam akiwa pamoja na viongozi mbalimbali kutoka nje na ndani ya nchi
Rais Dk. Jakaya Kikwete kulia akipokea Gwaride la Heshima lililpokuwa likipita mbele yake wanaofuatia katika picha ni Rais wa Zanzibar Dk. Mohamed Shein, Rais wa Namibia Mh. Ifikepunye Pohamba na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiwa katika maadhimisho hayo
Vijana wa chipukizi wakionyesha michezo na ujumbe mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo.
Hapa wakionyesha ukakamavu wao huku wakiwa wameshika silaha.
Kikosi cha wanaanga Jeshi la wananchi JWTZ kikitoa heshima kwa gwaride kali mbele ya Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jakmhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete
Kikosi cha ardhini Jeshi la wananchi la Tanzania JWTZ kipita kwa gwaride la heshima mbele ya Rais Dk. Jakaya Kikwete.

Sunday, December 9, 2012

NIYONZIMA AONGEZA MKATABA WA MIAKA 2 YANGA KWA DOLA 70,000 NA MSHAHARA WA DOLA 3,000


Habari na Picha kwa hisani ya Shaffih Dauda
Zikiwa zimepita siku kadhaa za mazungumzo juu ya kuongezwa kwa muda wa mkataba kiungo mshambuliaji wa Dar Young African - Haruna Niyonzima, hatimaye siku ya jana klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati imefanikiwa kukubaliana kimsingi na mchezaji huyo kumuongezea mkataba mpya.

Taarifa rasmi nilizozipata ni kwamba Haruna Niyonzima ambaye amebakiza miezi sita katika mkataba wake na Yanga amekubali kuongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuichezea Yanga.


"Niyonzima alikuja Tanzania siku tatu zilizopita kwa ajili ya mazungumzo na uongozi wa Yanga, lakini mwanzoni hawakupata muafaka, ila hatimaye jana alikubaliana na Yanga kuongeza mkataba wa miaka miwili kwa kulipwa dola 70,000 kama fedha ya usajili na mshahara wa dola 3,000 kwa mwezi," kilisema chanzo cha habari kilichokuwa karibu na uongozi wa Yanga.

ULIMWENGU WA HABARI: MAGAZETINI LEO

SWAHILI FASHION WEEK BAAB KUBWA!

Kama wewe ni mpenda mitindo basi jionee mwenyewe jinsi models walivyoonekana vizuri katika Ukumbi wa Golden Tulip ikiwa ni maonesho kwaajili ya wabunifu wachanga na waliobobea kuweza kutafuta masoko ya nje, ikifanya na USAID COMPETE shirika linalokuza vipaji vya watu mbalimbali.




 

AJALI YATOKEA MLIMA KITONGA IRINGA

Habari na Picha kwa hisani ya Francis godwin

Ajali yasababisha msongamano wa magari katika Mlima Kitonga barabara kuu ya Iringa -Mbeya baada ya lori kuanguka katika  eneo hilo .kutokana na ajali hiyo baadhi ya mabasi ya abiria  yanayokwenda Dar na kutoka mikoa ya kusini yalikwama kwa muda mchana  wa  leo hadi lori hilo  lilipovutwa  eneo hilo hakuna aliyepoteza maisha

Saturday, December 8, 2012

JIPANGE WOMEN GROUP YAENDELEA NA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI


SUALA la elimu ya Ukimwi nchini limetakiwa kutiliwa mkazo kutokana na ugonjwa huo kuendelea kuwa tishio kwa wananchi wengi wa Tanzania.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Jipange Women Group Bi. Janeth Mavinza wakati wa kutoa huduma ya kupima Ukimwi eneo la Ujiji lililopo Mwananyamala, jijini Dar es salaam.
Bi. Janeth Mavinza Mwenyekiti wa Jipange Women Group akiongea na waandishi wa habari katika eneo la ujiji, Mwananyamala, jijini Dar es salaam.
Bi. Janeth Mavinza amesema licha ya wanawake hao kujishughulisha na ujasiliamali, pia wanatoa msaada wa upimaji Ukimwi kwa hiari.

Kikundi hicho cha Jipange Women kina asili ya VICOBA ambapo kimewakutanisha akina mama wajasiliamali ili kuleta maendeleo ya kijamii.


Badhi ya wananchi waliojitokeza kushiriki katika mchakato huo
Bi. Frola Mwakajinga - Katibu
Bi. Frola Mwakajinga kama katibu wa Jipange Women Group akaeleza umuhimu wa jumuiya hiyo, huku akisisitiza wanawake kujiunga pamoja na kutatua matatizo yao kupitia vikundi mbalimbali wanavyoviunda, lakini kikubwa ni kufanya kazi kwa bidii.

Wananchi nao walijitokeza katika kupata huduma hiyo ya kupima kwa hiari huku wengi wakizitaka taasisi nyingine za Afya kutoa huduma hiyo kwa watu waliopopembezoni mwa mji kutokana na ukweli kwamba katika maeneo hayo huduma hii ni duni sana.

Friday, December 7, 2012

WAMA WATOA VITANDA 80 MUHIMBILI


Mwenyekiti wa Wama mama Salma Kikwete akikata utepe kama ishara ya kukabidhi vitanda 80 kwa uongozi wa Hospitali ya Muhimbili leo, kulia ni Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi na kushoto ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili Dk Marina Njelekela.
PICHA NA FULLSHANGWEBLOG.COM

Mama Salma Kikwete akisoma hotuba yake mara baada ya kukabidhi vitanda 80 katika hospitali ya Muhimbili leo (kushoto) ni Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi na kulia ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili Dk Marina Njelekela.
Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi akisoma hotuba yake.







Baadhi ya Waganga na wauguzi wa hospitali ya Muhimbili wakishuhudia tukio hilo.
Mama Salma Kikwete akiongozwa na Mkurugenzi wa Hospitali ya Muhimbili Dk. Marina Njelekela kushoto wakati akielekea wodini kuwatembelea wagonjwa, kulia ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi na katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi.
Mama Salma Kikwete akimjulia hali Anna Razalo kutoka Nyegezi Mwanza mmoja wa wagonjwa wa moyo aliyelazwa hospitalini hapo.



Pichani ni moja ya kitanda kilichotolewa kama msaada na WAMA

ZILIZOSOMWA ZAIDI