NYUMBANI KITAIFA

Ulimwengu wa habari.

KATIKA BIASHARA

Ulimwengu wa habari.

MATAIFA MENGINE

Ulimwengu wa habari.

KATIKA BURUDANI

Ulimwengu wa habari.

MAAJABU DUNIANI

Ulimwengu wa habari.

Thursday, July 21, 2016

KALA JEREMIAH AFICHUA MAAJABU YA MTOTO HUYU ALIYEMSHIRIKISHA ‘WANA NDOTO’

ffff
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Kala Jeremiah anaendelea na nyimbo zake za kiuwanaharakati ambapo anatarajia kuachia wimbo wake mpya ‘Wana Ndoto’ aliomshirikisha binti mdogo.
Rapper huyo alisema wimbo huo unazungumzia maisha ya jamii pamoja na watoto wadogo ambao wanandozo za kufanya mambo fulani katika maisha yao.
Jumatano hii, Kala ameamua kuweka wazi uwezo na binti huyo ambaye amemshirikisha katika wimbo huo.
“Nimewahi kukutana na watoto wengi wenye vipaji lakini sijawahi kukutana na mtoto mwenye kipaji cha hali ya juu kama huyu mtoto,” aliandika Kala kupitia instagram.
Aliongeza, “Anauwezo mkubwa sana wa kuimba na ana akili nyingi sana. Mungu kambariki sana.
Ukitaka kuamini hayo subiri tarehe 26/7 /2016 siku ambayo ‪#‎wanandoto‬ inatoka. huyu ndiye kaimba kiitikio. wakati unaendelea kusubiri Wana Ndoto unaweza kwenda youtube na kuandika miriam chirwa utaona mambo yake. na utaamini ninachokisema,”

CHECK VIDEO MPYA YA EMMANEM ON AIR – CHUMA YAO

Video ya rapper Emmanem On Air ya wimbo wake Chuma Yao.
Video imeongozwa na Hobo Cinemax.

EXCLUSIVE: BABUTALE AELEZA YAKE KUHUSIANA NA AMRI YA MAHAKAMA YA KUKAMATWA NA KUMLIPA SHEIKH MILIONI 250

13525399_932827003529799_1639302313_n
Meneja wa Tip Top Connection na wa Diamond Platnumz, Babutale anakabiliwa na mtihani mzito baada ya mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam kutoa hati ya kukamatwa kutokana na kudaiwa kutotii amri iliyomtaka amlipe Shekh Hamis Mbonde, shilingi milioni 250.
Kwa mujibu wa habari iliyoandiwa na gazeti la Mwanahalisi Jumanne hii, Tale anatakiwa alipe kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa kudaiwa kuvunja mkataba kati yake na Sheikh Mbonde wa kuuza na kusambaza nakala za mawaidha (DVDs) bila ridhaa ya sheikh huyo.
Tale na kaka yake Idd waliamriwa na mahakama hiyo kulipa kiasi hicho Februari 18 mwaka huu huku hati ya kukamatwa kwao ilitolewa July 8.
Mahakama ilitoa maelekezo kwa kamanda wa polisi kanda ya Ilala kuwa hadi Jumanne hii, July 19 wawili hao wawe wamekamatwa na kupandishwa kizimbani kujitetea kwanini wasipewe adhabu kwa kukiuka amri ya mahakama.
Hati nyingine ilitolewa Jumanne hii kwaajili ya kukamatwa kwa Babutale. Bongo5 imezungumza na Tale ambaye amedai kuwa makubaliano hayo yalifanywa baina ya sheikh huyo na marehemu kaka yake, Abdu Bonge na kwamba yeye hahusiki.
“Mimi na marehemu brother yangu tulifungua kampuni ya Tip Top Connection pamoja, mimi nifanye muziki yeye anisaidie.. Alipoona nimesogea akaona aachane na mimi ili afanye movie. Kwahiyo hakuwa anajua mimi ninachokifanya kwenye muziki, mimi pia sikuwa najua anachokifanya kwenye movie, imeenda akawa anafanya movie, sijawahi hata kushiriki hata kwa njia ya kuonekana location, hata kukaa nao kuongea nao lolote au kusainisha nao mkataba, so I know nothing,” amesema Tale.
“Mwaka juzi wakati nipo Uingereza yule Mzee akasikika kwenye U Heard kwamba anaidai Tip Top Connection milioni 50. Soudy Brown alimhoji akamuambia unamjua Babutale, akasema namjua lakini sijawahi kuongea naye hata siku moja. Akapeleka kesi mahakamani wakati brother yupo hai baadaye akaja akawa amefariki mimi nikawa sijui tena kinachoendelea. Kumbe yule mwanasheria alikuwa na marehemu brother na yule mzee wanakutana mahakamani. Mwaka huu kama mwezi mmoja uliopita akanipigia mtu simu, simu yangu napigiwa na watu wengi sana hii ‘mimi mwanasheria, unashtakiwa kwa kosa la kumdhulumu mtu kazi.’ Nikamuambia hizi kazi alikuwa akisimamia marehemu brother yangu kwahiyo story unazoniletea mimi unanirusha roho. Nikamwambia mimi naishi maisha yangu sijui kinachoendelea na sijawahi kujihusisha na chochote na hata huyo sheikh kama ana sehemu yoyote ambayo ameona kuna jina langu nimesaini naye niko tayari hata akisema ananidai,” anasisitiza.
“Kwahiyo wakati wanazunguka na kesi yao wakapita Brela kuchunguza hii kampuni wako nani na nani? Wakagundua kuna marehemu Abdul Bonge, mimi hapa na brother yangu mwingine lakini hawajui labda kwamba sisi tuligawana kila mtu na majukumu yake kwasababu kila mmoja alikuwa anafanya kile ambacho anakiweza.”
“Kwahiyo wameenda mahakamani wamepata barua wanikamate kwasababu mimi ninadaiwa. Mimi niko nyumbani wamekuja kugonga nyumbani kwangu kama majambazi. I was like wewe unakuja unajua hapa kwa nani? Mbona unataka kuniharrass rafiki yangu? Wewe unakuja kumkamata mtu usiyemfahamu! ‘Wewe si Tale’ walikuwa hawajui kama mimi ndio Babutale. Kama wao wananitaka wangeniambia mimi nipo Oysterbay polisi hapa, hawajaja. Mimi asubuhi ndio nikatoka nikaenda kumfuaya yule mwanasheria ambaye anasimamia kesi kuaniambia kuna nini naona kama watu wananitumia meseji kwamba nimeshtakiwa, akanihadithia in and out.”
“Tangu nijue kila kitu leo nina siku ya nne, I know nothing, sijawahi kumuona huyo mzee hata akitokezea sehemu simjui kwa sura. Lakini sasa yule mwanasheria wa yule mzee anasema Babutale ana hela, tukimshtaki Babutale atauza nyumba au watu watamchukua au tukimdhalilisha kwenye mitandao ataona aibu atataka kulipa. Vaa kiatu changu, wewe ni sehemu gani unalipa hapo? Sijui chochote, lakini wao wanaamini kwasababu mahakama imewaamuru nimewalipe milioni 250 na wanaamini mimi nina hela basi nitawalipa tu, haiwezekani,” amesema Tale.
Hata hivyo meneja huyo bado yupo njia panda kutafuta njia ya kujinasua kutoka kwenye hukumu hiyo nzito.
“Sijajua nini nitakachofanya, I know nothing,” anasema. “Anachokifanya ameamua kunichafua bila sababu, hajui kwamba mimi najianda kuwa waziri wa hii nchi na kuwa mbunge, anajiandaa kunifanya nionekane tapeli halafu ni mtu wa dini labda.”
Marehemu Abdul Bonge aliyefariki March 2015 na Mbonde waliingia makubaliano hayo June 16, 2013 kufanya biashara ya kurekodi mawaidha na kutengeneza nakala DVDs na kuziuza nchini.
Pia alimuahidi kumjengea nyumba, kumnunulia gari na kuitangaza kazi yake na kumpa shilingi milioni mbili na kumnunulia kanzu na kofia (baraghashia) na kurekodi DVDs zenye ujumbe Uzito wa Kifo, Fitina Juu ya Wanawake, Umuhimu wa Swala, Mwanadamu Yumo Ndani ya Hasara na Maadui wa Uislam, kwa mujibu wa Mwanahalisi.
Kwa mujibu wa Jaji Augustine Jangwa, makubaliano ya awali yalikuwa kurekodi halafu baadaye wakubaliane kuhusu bei na jinsi ya kuziuza na kwamba badala yake waliziuza na kuzisambaza nakala hizo na kujipatia faida bila kumshirikisha Mbonde ambaye alitumia ujuzi wake.
Awali Mbonde kupitia wakili wake Muhingo, Gwamaka Mwaikugile na Clement Kihoko alitaka alipwe shilingi milioni 700 kama fidia ya kuvunja makubaliano yao.
#Mwanahalisi Online

Wednesday, July 13, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA MPANGO WA UGAWAJI WA MADAWAJI KWA MAJIMBO MBALIMBALI NCHINI *PICHAZ*


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la Ilala Mh. Idd Azzan Madawati yaliyotolewa na Ofisi ya bunge kwa ajili kwa niaba ya wabunge waliopata mgao huo katika awamu ya kwanza.Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao, katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua madawati katika mfano wa Darasa wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao, katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam. Anayemfuata ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa na kulia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na baadhi ya watoto wa shule ya msingi bunge wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao, Leokatika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waheshimiwa wabunge waliohudhuria hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi kutoka shule ya msingi bunge iliyopo Jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Temeke Abdallah Diwani, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Charles Kuyeko, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mstahiki Meya Isaya Mwita na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amezindua mpango wa ugawaji wa madawati yanayotengenezwa kutokana na fedha zilizotolewa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kubana matumizi katika bajeti yake.

Uzinduzi huo umefanyika leo tarehe 13 Julai, 2016 katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam ambapo Rais Magufuli amekabidhi madawati 537 kwa mbunge wa jimbo la Ilala Mheshimiwa Mussa Azan Zungu kwa niaba ya wabunge wa majimbo yote ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar ambayo yatagawiwa idadi hiyohiyo ya madawati kwa kila jimbo.

Madawati hayo 537 ni sehemu ya madawati 61,385 ambayo yametengenezwa katika awamu ya kwanza na yatafuatiwa na madawati mengine 60,000 yatakayogawiwa katika awamu ya pili na yote kwa ujumla yatagharimu shilingi bilioni 4 ambazo zilitolewa na Bunge tarehe 11 Aprili, 2016 baada ya kubana matumizi katika bajeti yake, ikiwa ni kuitikia wito wa Mhe. Rais John Pombe Magufuli.

Mikoa itakayonufaika katika awamu ya kwanza ya ugawaji wa madawati hayo ni Dar es salaam, Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, Rukwa, Katavi, Unguja, Pemba na Tanga.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Magufuli amewashukuru na kuwapongeza wabunge kwa kutoa mchango huo na pia amewapongeza wadau wengine ambao wameitikia wito wake wa kuchangia madawati kwa lengo la kuondoa tatizo la wanafunzi kukaa chini.

Rais Magufuli amesema baada ya kuanza kutekeleza ahadi ya kuondoa ada kwa shule za msingi na sekondari, idadi ya wanafunzi waliojiandikisha kuanza darasa la kwanza imeongezeka kutoka wanafunzi 1,282,100 hadi kufikia wanafunzi 1,896,584 sawa na ongezeko la asilimia 84.5 hali iliyosababisha upungufu wa madawati 1,400,000 lakini tatizo hilo limetatuliwa kwa kiasi kikubwa ambapo mpaka sasa zaidi ya madawati 1,000,000 yametengenezwa.

Aidha, Dkt. Magufuli amelitaka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Jeshi la Magereza kuongeza kasi katika utengenezaji wa madawati ili yakamilike haraka na kuanza kutumika.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Wabunge wa kamati ndogo ya tume ya huduma za bunge, Viongozi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Magereza pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Bunge.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Julai, 2016

Tuesday, July 12, 2016

RAIS MUSEVENI WA UGANDA ASIMAMISHA MSAFARA KUPOKEA SIMU *PICHAZ*

Rais wa Uganda bwana Yoweri Kaguta Museveni alizua kihoja katika kijiji kimoja karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania
Je ushwahi kupokea simu ya dharura ?
Je wewe hujitenga vipi na watu waliokaribu nawe ima ni mkeo ama hata wafanyakazi wenza iliupokee simu ya kibinafsi?
Na je katika enzi hizi za simu za kisasa au Smartphone wangapi wetu wanatumia simu za kale zisizo na touchscreen ?
Haya basi ,
Museveni hata aliwapungia mkono wapita njia
Hayo sio maswali ya kipima joto,,,la!
Rais wa Uganda bwana Yoweri Kaguta Museveni alizua kihoja katika kijiji kimoja karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania aliposimamisha msafara wake wa magari iliapokee simu faraghani.
Amini usiamini Rais Yoweri Museveni, alishuka kutoka kwenye gari lake rasmi akachukua kiti chake na kukiweka kando kando ya barabara mpya ya Isingiro ikipitia kijiji hicho cha Kyeirumba hadi Tanzania na kupokea simu faraghani.
Wenyeji walifurahia kuwa na mgeni ambaye hawakumtarajia
Mzee Museveni kama vile baba wa taifa alitumia muda wake kufanya shughuli hiyo huku akiwapungia mkoo wapita njia.
Baada ya dakika 30 hivi raia wa kijiji hicho walishangaa kuwa miongoni mwa maafisa wakuu serikalini.
Wenyeji walikuwa na la kumweleza kiongozi huyo wa taifa
Ilikuwa ajabu sana kwao kumuoana Museveni akiwa ameketi barabarani.
Waganda katika mitandao ya kijamii wamesambaza picha hiyo ya rais museveni akizungumza kwa simu ambayo inaonekana kuwa sio ya kisasa.
Je wewe hujitenga vipi na watu waliokaribu nawe ima ni mkeo ama hata wafanyakazi wenza iliupokee simu ya kibinafsi?
Wengine wanamkejeli kwa kuhofia kudukuliwa huku wengine wakimgoa kwa kuketi barabrani
''kwani hangeweza kupokea simu yake ndani ya gari lake ?
''ni siri gani hiyo ambayo hakutaka hata walinzi wake wasikie,
''Ama ilikuwa ni #Besigyexit ? wakizungumzia kuachiliwa kwa dhamana kwa kiongozi wa upinzani Kizza Besigye.
#BBC Swahili

VIJANA WA CHADEMA WATII AGIZO LA MBOWE..VIONGOZI WAO KUFIKISHWA MAHAKAMANI LEO

JESHI la Polisi limekwama kuwafikisha mahakamani viongozi wanne wa Taifa wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), baada ya kukosea hati ya mashtaka.

Wanaoshikiliwa ni Mwenyekiti wa Taifa, Patrobas Katambi, Katibu Mkuu, Julius Mwita, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Joseph Kasambala na Mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya, George Tito.

Akizungumza jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema makosa yametokea wakati wa uandaaji wa hati ya mashtaka.

 “Mahojiano yameisha, charge sheet (hati ya mashtaka) ikaandaliwa, lakini ikarudishwa tuifanyie marekebisho. Muda umepita wa Mahakama watapelekwa kesho (leo),” alisema.

Hata hivyo, alisema kesi hiyo haina dhamana kwa upande wa kituo cha polisi na hivyo kuwalazimu watuhumiwa hao kuendelea kukaa rumande.

 “Wasubiri kesho (leo) wataka- poenda mahakamani kama wataamua kuwapa dhamana,” alisema Mambosasa.

Kuhusu baadhi ya watuhumiwa hao kugawanywa katika selo tofauti za Chamwino na wengine kuachwa Kituo Kikuu cha Polisi, Mambosasa alisema huo ni utaratibu wa kawaida ambao unalenga kupata maelezo ya kila mmoja.

“Hayo ni mahojiano tu ili kila mmoja upate anasema nini ndipo unawaweka sehemu tofauti. Hizo ni taratibu za mahojiano ili wasiendelee na mawasiliano,” alisema.

Makamu Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi alisema kisheria watuhumiwa hawatakiwi kukaa rumande kwa zaidi ya saa 24.

“Cha kusikitisha siku ya leo (jana) ambayo walisema wangewaleta mahakamani kwa kile wanachoamini wametenda kosa, lakini hadi sasa muda wa mahakama unaisha viongozi wetu hawajaletwa,”alisema na kuongeza:

“Na sisi tunataka kuondoka ili tuone taratibu nyingine ambazo zinaweza kutuhakikishia  usalama wa viongozi wetu. Hadi sasa viongozi wetu hawajaletwa mahakamani.”

Alisema hata kama polisi wanawaona viongozi wao wanamakosa, kisheria hawawezi kukaa na mtu kwa muda wa siku tatu bila kumfikisha mahakamani.

Alisema utendaji wa polisi nchini ni tofauti na wa nje ya nchi ambapo kwa nchi za wengine, polisi ni sehemu ya huduma na si ya mabavu.

 Alisema hali hiyo inaleta kadhia na masumbuko kwa Watanzania na hivyo kupunguza imani yao kwa jeshi hilo.

 Wakili wa watuhumiwa hao, Fred Kalonga alisema wamekuwa na wateja wao tangu siku walipokamatwa kwa kuhakikisha wanahojiwa kwa mujibu wa sheria.

 “Kwa mujibu wa ahadi za polisi kuwa leo (jana) wanaletwa mahakamani. Kuanzia saa 1.30 asubuhi tuko mahakamani na sasa inakwenda saa 9.30 alasiri hakuna mtuhumiwa aliyeletwa. Kimsingi muda wa mahakama umeisha,” alisema.

Alisema yeye na wakili mwenzake, Azack Mwaipopo walikuwa wanakwenda kufuatilia taratibu nyingine za kisheria za kuwawezesha kupata dhamana.

“Tunakwenda kufuatilia taratibu nyingine lakini sisi tupo tayari muda wowote wakiletwa tutawadefend (tutawatetea) kwasababu tunaamini kwa mujibu wa maelezo ya wateja wetu wapo sahihi kuliko tuhuma zinazowakabili,” alisema.

Wanachama wa Chadema walikuwa katika viwanja vya mahakama tangu saa 2.00 asubuhi hadi saa 9.30 alasiri baada ya kuelezwa na wakili wa watuhumiwa kuwa viongozi wa Bavicha hawatapelekwa mahakamani tena.

Viongozi hao walikamatwa Ijumaa usiku katika baa ya Capetown walipokwenda kunywa na kula chakula. Wanadaiwa kwa tuhuma za kukusudia kuikashfu Serikali.

Akizungumzia mpango wa vijana wa Chadema kuzuia mkutano wa CCM utakaofanyika Julai 23 mjini hapa, Sosopi alisema wanaiheshimu kauli ya Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe ya kuwataka kutokwenda kuzuia mkutano huo.

“Tunaiheshimu kauli ya mwenyekiti na tunatambua kuwa vijana wengi nchi nzima wamejiandaa kwenda kuzuia mkusanyiko huo, lakini sasa tunashughulika na hili la viongozi wetu kukamatwa kwanza,”alisema.


Alisema baada ya viongozi wao kupata dhamana wataitisha kikao cha Kamati ya Utendaji ya Bavicha haraka ili kujadili suala hilo na watatoa msimamo kama wanakuja na mkakati mwingine ama kuendelea na huohuo

WAUAJI 30 WA ALBINO NA VIKONGWE KUNYONGWA

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema jumla ya watuhumiwa 30 wa mauaji ya vikongwe na wenye ulemavu wa ngozi (albino) nchini, wamehukumiwa kunyongwa, baada ya kupatikana na hatia ya mauaji hayo.

Dk Mwakyembe amesema pia kuwa serikali itaendelea kutoa adhabu kali kwa watu watakaobainika kuendelea kuhusika na mauaji ya watu hao ili kumaliza tatizo hilo, ambalo limeipaka matope Tanzania kwa kuonekana sio kisiwa tena cha amani. Waziri huyo alisema hayo mjini Shinyanga jana, alipofanya ziara yake ya kikazi.

Alisema katika miaka ya hivi karibuni tatizo la mauaji ya wenye ualbino na vikongwe yamepungua nchini na kwamba watahakikisha wanayakomesha kwa kutoa adhabu kali kwa wauaji.

“Tatizo hili la mauaji ya vikongwe na albino linatutia sana doa nchi yetu kimataifa ambayo imekuwa ikisifika kwa amani na utulivu, hivyo natoa mwito kwa wananchi waachane na mauaji ya watu hawa wasio na hatia pamoja na mahakama zifanye kazi kwa kutoa hukumu za haraka kwa watu watakaohusika na mauaji hayo,” alisema Dk Mwakyembe.

Hata hivyo, Dk Mwakyembe alisema serikali itaanza mikakati ya kujenga mahakama za mwanzo kwa kila kata nchi nzima ili kuondoa misongamano za kesi mahakamani na kukarabati majengo ya mahakama ambayo yamechakaa.

Aliwataka wakuu wa wilaya, waunde kamati za maadili ya wilaya.
Akisoma taarifa ya mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainabu Telack, alitaja changamoto ambazo zinawakabili kuwa ni uchakavu wa majengo ya mahakama, uhaba wa mahakimu na magereza ya Shinyanga na Kahama kuwa finyu na hivyo kusababisha mlundikano wa wafungwa.

KITUO CHA DK. MWAKA CHAFUTIWA USAJILI, WENGINE KUSIMAMISHWA MIEZI 6 NA KUPEWA ONYO KALI

BARAZA la Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini, limekifutia usajili wake wa kutoa huduma za kitabu, Kituo cha Tiba Asilia cha ForePlan Kliniki kilichopo Ilala Bungoni jijini Dar es salaam, kinachomilikiwa na Dkt. Juma Mwaka maarufu kama Dkt. Mwaka, kwa madai kuwa kimekiuka taratibu za kitabu za tiba mbadala.

Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Dkt. Edmund Kayombo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Ukumbi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Akizungumza jijini Dar es salaam leo katika Mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Baraza hilo, Dk. Edmund Kayombo amesema kuwa kufutiwa kibali cha Dk. Mwaka kunatokana na sababu nyingi ambazo amekuwa akikiuka licha ya kupewa maonyo na barua juu ya utoaji huduma zake.

Amesema sababu nyingine ni kuwa katika matangazo yake amesema anatoa tiba za kisasa wakati hiyo elimu hana ya kufanya huo.

Wengine waliofutiwa usajili ni Fadhaget Sanitarium kinachoendeshwa na Tabibu Fadhili Kabujanja pamoja na Mandai Herbal Clinic kinachoendeshwa na Tabibu Abdallah Mandai

Hata hivyo limetoa adhabu mbalimbali kwa kituo cha Aman Herbal Clinic kinachoendeshwa na Tabibu Esbon Baroshigwa, na Tabibu Castory Ndulu wa Kituo cha Ndulu Herbal Clinic wamepewa barua ya onyo.


Aidha wengine wamesimashwa kwa miezi sita ambao ni Tabibu John Lupimo wa Lupimo Suntarium Herbal Clinic pamoja na Tabibu Simon Rusigwa wa Sigwa Herbal Clinic.

WAKURUGENZI WATENDAJI WA HALMASHAURI, MIJI, MANISPAA NA MAJIJI 185 WALA VIAPO VYA MAADILI IKULU LEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Miji, Manidpaa na Majiji 185 kabla ya hawajakula kiapo cha maadili ya viongozi leo Ikulu jijini Dar es salaam. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Mkutano ulioitishwa  na Rais John Magufuli kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote za wilaya na baadhi ya Wakuu wa  wilaya  ikulu jijini Dar es salaam Julai 12, 2016.
Sehemu ya Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Miji, Manidpaa na Majiji 185 wakipata maelezo ya awali kabla ya kula kiapo cha maadili ya viongozi leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri, Miji, Manispaa na Majiji 185 wakila kiapo cha maadili ya viongozi leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Wakuu wa wilaya za Kongwa Mhe deo Ndejembi (kushoto), Siriel Shaidi Mchembe (DC Gairo) na Mhe. Geoffrey Idelphonce Mwambe (DC Manyoni) wa kila kiapo cha maadili ya viongozi leo Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kukosa kufanya hivyo na wenzao wiki iliyopita.
#Picha na Ikulu

BABY FUTURE AANZA KUMUITA MUME WA CIARA ‘BABA’ *VIDEO*

13652111_220707744990138_1412425769_n
Hivi karibuni Ciara alifunga ndoa na mchumba wake Russell Wilson nchini Uingereza. Na sasa mtoto aliyezaa na rapper Future ameanza kumuita Russell ‘Papa’ neno linalomaanisha ‘Baba.’
Video inayomuonesha mtoto huyo akimuita baba yake wa kufikia ‘Papa Russ’ imesambaa mtandaoni. Mtoto huyo anaonekana akimuomba busu Russell na yeye kumjibu ‘You’re so sweet.’
Hivi karibuni mahakama iliamua Ciara na Future wawe na haki sawa za kumleta mtoto wao aitwaye Future.
Wilson na Ciara walifunga ndoa wiki iliyopita.

Monday, July 11, 2016

COUPLE 10 ZA MASTAA WABURUDISHAJI ZENYE NGUVU ZAIDI TANZANIA – 2016 *PICHAZ*

13395089_214032905662116_1444251759_n
Tanzania imebarikiwa kuwa na tasnia ya burudani yenye watu wenye nguvu sana.
Lakini nguvu yao huwa maradufu pale wakiwa na uhusiano wa kimapenzi na mastaa wenzao. Ninakuletea orodha ya couple 10 za mastaa wa Tanzania zenye nguvu zaidi kwa sasa. Nguvu zao zipo kwenye lundo la mashabiki walionao, ushawishi wao, utajiri wao na wafuasi walionao kwenye mitandao ya kijamii. Wengi ni kutokana na jinsi walivyodumu kwa muda mrefu, kutumia brand zao kwa pamoja kujikuza na mambo mengine kibao.
1. Diamond Platnumz na Zari the Bosslady
13395089_214032905662116_1444251759_n

Himaya ya Diamond yenye utajiri unaokadiriwa kuwa zaidi ya shilingi bilioni 8 ina nguvu isiyoelezeka pale inapoungana na mwanamke aliyeachiwa utajiri mkubwa na ex wake na kujitengenezea himaya yake mwenyewe pia. Wanakaribia kufikisha miaka miwili sasa tangu wawe pamoja na ukikumbuka walivyoanza kwa kujiita ‘project’ hakuna aliyewahi kudhani kama wangeendelea kudunda hadi leo.
Sasa hivi ni wazazi wa mtoto wao mwenye miezi 11, Tiffah. Hii ni couple inayozungumzwa zaidi Afrika Mashariki, isiyokauka kwenye vichwa vya habari vya magazeti ya udaku kila iitwapo leo. Ni couple inayojadiliwa zaidi kwenye mitandao ya kijamii na lundo la wafuasi walio nyuma yao tayari kwa kumshambulia yeyote anaye hatarisha uwepo wake, linatisha. Kwa pamoja wana wafuasi kwenye Instagram zaidi ya milioni 4.2 huku mtoto wao akiwaongezea wengine 700k na kuwa na takriban milioni 5.
Pamoja na hivyo, hii ni couple isiyokaukiwa misukosuko na skendo kibao zikiwemo za Diamond kuwahi kudaiwa kuchepuka na mrembo wa video ya Kwetu ya Raymond hadi tetesi kuwa Zari hana maelewano mazuri na ndugu za mchumba wake. Zari pia amekuwa akiwekwa kitimoto kwa kuendelea kuwa na mawasiliano na ex wake, Ivan, kitu ambacho hakiepukiki sababu wana watoto watatu wa kiume waliozaa pamoja.
Pamoja na hivyo, bado wameendelea kuonesha kutoteteleka na dhoruba hizo na mashua yao inaendelea kukata mawimbi baharini na huenda Tiffah akaja kupata mdogo wake, huku pia uwezekano wa kufunga pingu za maisha siku za usoni ukiendelea kuwa mkubwa.

2. Idris Sultan na Wema Sepetu

Wema
Mshindi wa Big Brother Africa aliyegeuka kuwa milionea ndani ya miezi mitatu na Miss Tanzania 2006 na muigizaji maarufu zaidi wa filamu Bongo wanapounda umoja wa kimahaba, matokeo yake ni makubwa. Idris Sultan na Wema Sepetu wana nguvu kubwa ambayo couple pekee iliyo na cheche za kuwazidi ni hiyo ya juu.
Hata hivyo yote yanarudi na kuanzia nyuma tena. Wema alikuwa kwenye uhusiano maarufu na wa muda mrefu na Diamond ambao bahati mbaya pamoja na kuachana, hadi leo harufu za mahaba yao zimeendelea kuwanyemelea na kutengeneza chuki na upendo kwa pamoja.
Idris alijikuta akizidiwa na nguvu ya umaarufu wa uhusiano wao hadi kuapa kutouweka hadharani tena – kitu ambacho kinaonesha ni kigumu kukifanikisha. Wao pia walikaribia kufika kwenye hatua muhimu ya kupata mtoto – mapacha, lakini kwa maneno yao wenyewe, Mungu hakupenda iwe hivyo. Bado suala la Wema kutopata mtoto limeendelea kuwa kidonda kibichi kinachotoneshwa mara nyingi.
Idris na Wema wamepitia majaribu mengi ambayo wakati mwingine huyashindwa kuyahimili na kuachana, lakini hugundua bado wanapendana na kurudiana tena. Kwa mfano kipindi video ya Wema imesambaa mtandaoni akimbusu mwanaume mwingine, iliuvunja moyo wa Idris kiasi cha kuamua kulivua pendo – kwa muda.
Hivi karibuni pia baada ya Wema na Diamond kuonesha kuvunja uhasama wao, Wema kumtumia salamu za siku ya kuzaliwa Bi. Sandra (mama yake Diamond) Idris alitafsiriwa na wengi kujikuta njia panda kwa mtazamo kuwa hapewi heshima anayostahili na mpenziwe. Hata hivyo hakujali na kwa wale waliohudhuria show yao ya Black and Tie, mwishoni mwa wiki, walishuhudia jinsi njia hao walivyokuwa wakitembea kama kumbi kumbi – mapenzi tele.
3. Alikiba na Jokate Mwegelo
KIba
Pamoja na wao wenyewe kuendelea kukwepa kukiri hadharani kuwa ni mtu na mpenzi wake, ni kipofu pekee asiyeweza kutambua pendo zito lilivyowajaa, Alikiba na Jokate Mwegelo. Wamekuwa pamoja kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa kiasi ambacho uhusiano wao sio siri tena katika familia za pande zote mbili – ikiwa ni pamoja na Jokate kutambua na kujali uwepo wa watoto wa Alikiba.
Wamekuwa wakitengeneza headlines nyingi mno kwenye magazeti ya udaku kuhusu uhusiano wao lakini hadi sasa hawataki kuwapa kile mashabiki wao wamekuwa wakikiota kwa muda mrefu – kuuweka uhusiano wao wazi kama couple hizo juu.

Kitendo cha kuficha mahusiano yao si kigeni hata katika maisha yao ya nyuma. Pamoja na kuwahi kuwa na uhusiano na Hasheem Thabeet na kisha Diamond kwa muda mfupi, Jokate hajawahi kupendelea kuweka wazi maisha yake binafsi.
Alikiba pia vivyo hivyo, pamoja na kuwa na watoto watatu hadi sasa, kila mmoja na mama yake, hakuwahi kuwa mtu wa kuwaweka wazi wapenzi wake. Vyovyote ilivyo, mapenzi yao yanaonekana wazi kwa wale waliowahi kubahatika kuwaona wakiwa pamoja na pengine kuna siku wataamua kuuweka rasmi uhusiano wao kama mastaa wengine.
4. Jux na Vanessa Mdee
Jux and Vanessa Mdee
Iliwachukua muda mrefu sana Jux na Vanessa Mdee kukiri kuwa ni wapenzi. In fact, pamoja na kuamua kuuweka wazi, bado si watu wanaofurahia sana mada ya uhusiano wao. Wana takriban miaka miwili sasa tangu waanze kuwa pamoja.
Kuna wakati waliamua kuuweka wazi kidogo uhusiano wao kwa kuweka picha zao wakiwa kwenye mitandao ya kijamii, lakini sasa wameamua kuacha japo kwa walio karibu nao wanafamu jinsi wawili hawa wanavyopendana na kusaidiana katika kazi zao.

Kuna wakati pia Jux alimtumia Vee kwenye video yake lakini pia mara kibao Jux amekuwa karibu na mpenzi wake wakati akishoot video zake SA – mfano wakati akishoot video ya Never Ever.
Nina uhakika kuwa Jux ana ushindani mkubwa kuhakikisha kuwa Vee anaendelea kuwa wake daima na hii ni kutokana na umaarufu alionao Vanessa barani kote huku safari za nje zikiwa hazikauki. Jux pia kwa upande wake anafahamika kwa maisha ya kifahari aliyonayo na hivyo kujitengenezea sumaku inayovutia warembo wengi, achilia mbali maisha yake ya kusafiri mara kwa mara kwenda China masomoni.
Kwa namna yoyote ile, wawili hawa wanaonekana kuendana vyema na nina uhakika bado wana miaka mingi ya kuendelea kuwa pamoja.
5. Master J na Shaa
Master-J
Master J na Shaa walikutana takriban miaka kumi iliyopita. Shaa alikuwa msichana mdogo ambaye damu ya kufanya muziki ilikuwa ikichemka na kushinda shindano la Cocacola Popstars. Master J aliteuliwa kwenda nao Afrika Kusini kama producer wa kundi lililoanzishwa, Wakilisha. Baada ya kurudi, Shaa kwenda tena Marekani kusoma na kundi likavunjika, Shaa alirejea na kuwa chini ya MJ Records.
Sifahamu uhusiano wao kimapenzi ulianza lini lakini wana muda mrefu sana kwa sasa. Uhusiano wao umepitia majaribu mengi pia kuanzia Master J kutengana na mke wake aliyezaa naye watoto watatu warembo wa kike hadi Shaa kulalamikiwa kuwa sababu ya kuvunjika kwa ndoa hiyo. Master J amewahi kukiri mara nyingi kuwa kuvunjika kwa ndoa yake lilikuwa jaribu kubwa zaidi katika maisha yake. Hata hivyo yeye na Shaa waliendelea kuwa madhubuti na hivi karibuni walidai kuwa wana mpango wa hatimaye kufunga ndoa.

6. Barakah Da Prince na Naj

13628138_1240767765933440_485090523_n
Kupanda chati na kufahamika haraka kwa Barakah Da Prince hakujatokana na hits zake tatu pekee – Siachani Nawe, Nivumilie na Siwezi, bali jinsi anavyoitupa karata yake kwenye masuala yahusishayo moyo. Amewahi kuhusishwa kuwa na uhusiano na list ndefu ya mastaa wakiwemo Meninah, Linah, Agnes Masogange, Nisha na hatimaye sasa akiwa na Naj aliyemrasimisha zaidi.
Naj, historia yake yake naye ni ya kipekee. Hakupata jina kupitia hit single yake na Mr Blue ‘Please Don’t Go’ tu bali kwakuwa na uhusiano na rapper huyo aliyemtumia pia kwenye video ya hit single yake, Tabasamu.
Barakah amekuwa mpenzi wake wa kwanza tangu aliporejea kutoka Uingereza alikokuwa masomoni kwa miaka mingi. Kwa sasa penzi la msanii huyo mpya wa Rockstar4000 na Naj limezidi kupamba moto na hawaoni haya kueleza wazi wanavyopendana.
7. Majizzo na Lulu
13557244_171259513288748_1474298025_n
Nilianza kuona dalili za kuwepo uhusiano wa Majizzo na Lulu miezi kadhaa iliyopita wakati wa tuzo za Africa Magic jijini Lagos. Majizzo alimsindikiza muigizaji huyo ambaye jina lake halisi ni Elizabeth Michael na akawa bahati kwake kwasababu alishinda.
Baada ya hapo tetesi za uhusiano wao zikawa kubwa zaidi. Uhusiano wao sasa unaonekana kuwa wazi zaidi licha ya kuzungukwa na maneno ya hapa na pale hasa kutokana na Majizzo kuachana na mzazi mwenzake, Hamisa Mobetto. Warembo hao kwa sasa ni kama paka na panya na timu zao zimewahi kurushiana vijembe mtandaoni.
Bado hata hivyo Majizzo na Lulu hawajataka kuyaweka wazi mambo ya faragha mara kwa mara na hivyo kuwafanya wengi kutaka kuwachimba zaidi.
Umaarufu na ushawishi wa Lulu ukiunganishwa na sifa za ujasiriamali na utajiri alionao Majizzo (Dj maarufu aliyewika zamani) kwakuwa Mkurugenzi Mtendaji wa EFM unaifanya couple hii iwe na nguvu sana.

8. Harmonize na Jacqueline Wolper

e0ca9c67-c1e2-49d5-8fad-aef387a7d3b9
Harmonize ametoka kwenye maisha duni ya kulala stendi ya mabasi hadi kusaini label inayomilikiwa na msanii mkubwa Afrika. Hiyo haikutosha, alienda mbali zaidi kwa kuanzisha uhusiano na mmoja wa mastaa wakubwa wa filamu nchini na gwiji wa fashion, Jacqueline Wolper.
Hadithi ya uhusiano wao inavutia pia. Wolper aliwahi kuwa na uhusiano na Diamond ambaye leo hii wamebaki wakiitana ‘mkwe’ huku Harmonize akipewa baraka za kufaidi kilichowahi kuwa mali ya bosi wake. Uhusiano wao uliteka vichwa vya habari ndani ya muda mfupi. Wengi walidhani ni kiki lakini baada ya muda mfupi kila mmoja alishangaa jinsi walivyozama kwenye mahaba mazito.

9. Quick Rocka na Kajala

Kajala-na-Quick
Nimeanza kuusikia uhusiano wa Quick Rocka na Kajala muda mrefu sana. Wao pia hawakuwa tayari kuuweka wazi na waliendelea kukanusha kuwa pamoja kwa kipindi kirefu. Lakini kama wasemavyo kuwa penzi ni kikohozi kulificha huwezi uhusiano wao ulithibitishwa katika mazingira tofauti tofauti ikiwemo video aliyopost Quick akimbusu muigizaji huyo.
10. Nahreel na Aika
12543287_1125680584111594_2090272718_n
Nahreel na Aika wametoka mbali. Kutoka kusoma pamoja India wakiwa na kundi la Pah One, hadi kutengeneza si tu kundi maarufu Afrika Mashariki, Navy Kenzo bali pia kuanzisha studio na label yao, The Industry. Kwa wanaowafahamu, watakubaliana nami kuwa, Nahreel na Aika si tu wapenzi, bali pia ni mtu na mshkaji wake na partiners kibiashara wanaoelewana kinoma.

CHECK OUT VIDEO MPYA YA G NAKO FT NIKKI WA PILI - LAINI

Rapper wa kundi la Weusi G Nako ameachia video mpya ya wimbo “Laini”, akiwa amemshirikisha Nikki wa Pili. Video imeongozwa na Freeman Richard.

ZILIZOSOMWA ZAIDI