Tuesday, July 12, 2016

BABY FUTURE AANZA KUMUITA MUME WA CIARA ‘BABA’ *VIDEO*

13652111_220707744990138_1412425769_n
Hivi karibuni Ciara alifunga ndoa na mchumba wake Russell Wilson nchini Uingereza. Na sasa mtoto aliyezaa na rapper Future ameanza kumuita Russell ‘Papa’ neno linalomaanisha ‘Baba.’
Video inayomuonesha mtoto huyo akimuita baba yake wa kufikia ‘Papa Russ’ imesambaa mtandaoni. Mtoto huyo anaonekana akimuomba busu Russell na yeye kumjibu ‘You’re so sweet.’
Hivi karibuni mahakama iliamua Ciara na Future wawe na haki sawa za kumleta mtoto wao aitwaye Future.
Wilson na Ciara walifunga ndoa wiki iliyopita.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI