NYUMBANI KITAIFA

Ulimwengu wa habari.

KATIKA BIASHARA

Ulimwengu wa habari.

MATAIFA MENGINE

Ulimwengu wa habari.

KATIKA BURUDANI

Ulimwengu wa habari.

MAAJABU DUNIANI

Ulimwengu wa habari.

Friday, January 6, 2017

MEEK MILL AMCHANA NICKI MINAJ BAADA YA KUMWAGANA

Muda mfupi baada ya Nicki Minaj kutangaza kupitia Twitter kuwa ameachana na Meek Mill, rapper huyo amemchana demu wake huyo wa zamani kwenye Instagram.
Alhamis hii, Meek aliweka picha Instagram ya viatu vyeupe brand ya Giuseppe Zanotti zenye mistari ya dhahabu na kuandika, “If you walk out don’t wear these, they wack.”


Viatu alivyoviponda Meek ni vile ambalo Nicki Minaj alivivaa kwenye video ya wimbo wa mwaka 2013 alioshirikishwa na Ciara, I’m Out.
Wimbo huo una mashairi ya Minaj yanayosema, “You gon’ play me? / On Instagram, ni**as trying to shade me / But your bitch at home trying to play me.”

ANGALIA *PICHAZ* ZA JENNIFER NA PATRICK WA KANUMBA WALIVYOKUWA WAKUBWA

HUENDA ukakutana barabarani na Hanifa Daud ‘Jennifer’ pamoja na Othman Njaidi ‘Patrick’ ambayo ni zao la marehemu Steven Kanumba na usiwafahamu kwa jinsi walivyokuwa wakubwa.
Vijana hao wawili walifanya vizuri ndani ya filamu ya Uncle JJ pamoja na This Is It wakiwa na marehemu Steven Kanumba.
 Jennifer ambaye mwaka 2014 alionekana kwenye filamu ya Zena na Betina ya Salma Jabu aka Nisha, amehitimu kidato cha nne mwaka huu.

Kwa upande wa Patrick 2016 alihojiwa na mtandao mmoja wa habari nakudai hana mazuka wa kuigiza kwa sasa kama zamani.
Angalia picha zao hapa.








Q CHIEF AZUNGUMZIA KWANINI NGOMA ZAKE HAZIFANYI VIZURI PAMOJA NA MAPUNGUFU YA LABEL YA Q MHONDA

Q Chief akiwa na Mkurugugenzi wa Qs Mhonda Entertainment
Msanii mkongwe wa muziki Q Chief amedai kuwa kuna mambo ambayo anakosea kwenye muziki wake ndiyo maana ngoma zake kadhaa alizoziachia hivi karibuni zimeshindwa kufanya vizuri zaidi kama alivyotarajia.
Muimbaji huyo ambaye yupo chini ya label ya Qs Mhonda Entertainment, ameiambia Bongo5 kuwa hali hiyo imemfanya akae yeye pamoja na uongozi wake ili kulitafuta ufumbuzi suala hilo.
“Baada ya kufanya ngoma kadhaa nimeona kuna ulazima wa kukaa chini na uongozi wa management yangu na kuisukuma ijisukume zaidi kunisukuma kwa maana thamani ya uwekezaji wa audio na video unatakiwa kuwa sawa au zaidi na thamani na promotion pamoja na maisha halisi ya msanii ambayo anatakiwa kuishi,” alisema Q Chief.
Aliongeza, “Kwa hiyo mwaka 2017 ni mwaka ambao nataka kufanya mabadiliko makubwa sana, lakini kabla ya yote nataka marekebisho katika mkataba wangu na Q Mhonda kwa sababu una mapungufu mengi sana, na ningependa kuyarekebisha kwa lengo la kuweka mambo sawa,”
Pia muimbaji huyo amewashukuru mashabiki wa muziki wake kwa kuonyesha mapokezi mazuri katika wimbo wake mpya alioshirikiana na Patoranking wa Nigeria.

RIYAD MAHREZ ATUMA UJUMBE KWA MASHABIKI BAADA YA KUSHINDA TUZO

NI furaha kwa kila mtu pindi mchango wake unapoonekana na kupewa zawadi – ndicho kilichomtokea Riyad Mahrez usiku wa Alhamisi hii baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa kuwabwaga washiriki wengine akiwemo Pierre-Emerick Aubameyang na Sadio Mane.
Mahrez ambaye ni mchezaji wa Algeria amewashukuru mashabiki wote duniani kutokana na kuwa na msimu mzuri kwa mwaka jana na kufanikiwa kuisaidia timu yake ya Leicester City kushinda taji la ligi kuu ya Uingereza.
Kupiti kwenye mitandao yake ya kijamii, mchezaji huyo ameandika, “African ballon d’or … I thank everyone who supporte me around Africa and around the world .”
Hii ni tuzo ya tatu kubwa kushinda kwa mchezaji huyu baada ya ile ya ‘Mchezaji bora wa mwaka ya chama cha wachezaji soka ya kulipwa Uingereza (PFA) na ‘BBC African Player of the Year’.

ANGALIA *PICHAZ&VIDEO* ZA WACHEZA DANSI 50 WALIOFUNGA MTAA KWA KUTUMBUIZA JUU YA MAGARI KUSHEREHESHA MAZISHI YA MWANASIASA TAIWAN

WACHEZA DANSI wa kike kwenye kumbi za usiku wapatao 50, wakiwa wamevalia vivazi vyeusi wamewaacha na mshangao wapita njia wakati wakiusindikiza mwili wa mwanasiasa mmoja aliyefariki mwezi Decemba nchini Taiwan.

Kwenye msafara wanawake hao wakiwa juu ya magari ya aina ya “Jeep”, yenye rangi tofauti walikuwa wakicheza na kuimba na kusababisha foleni kubwa ya magari barabarani na watu wengi kubaki wakiwashangaa, kwa kuwa ni kinyume na tamaduni za huko.
Waendesha pikipiki nao waliufuatilia msafara wakiwashangaa wanawake hao. Familia ya mwanasiasa huyo imesema, marehemu Tung Hsiang aliagiza kufanyika namna hiyo, kwa kuwa alipendelea mambo kama hayo.
Angalia Picha zaidi hapa chini:



MAREKANI YAENDELEA NA MPANGO WA KUWAHAMISHA WAFUNGWA TOKA GUANTANAMO BAY

Mmoja kati ya wafungwa waliohamishwa kutoka Guantanamo Bay akisalimiana na ndugu zake
MAREKANI imewaachia baadhi ya wafungwa wa Yemen waliokuwa wakishikiliwa katika gereza la Guantanamo Bay nchini Cuba.
Makao makuu ya Pentagon yamethibitisha kuwahamisha wafungwa hao na kusema kuwa kwa sasa ni wafungwa 55 wamebakia katika gereza hilo. Mwandishi wa AFP amedai kuwa aliwaona wafungwa wanne wakishuka katika uwanja wa ndege wa Riyadh ambao umezoeleka kwa kutua viongozi wakubwa.
Baada ya kuwaona ndugu zao mmoja wa ndugu wa wafungwa hao, Mohammed Bawazir alisema, “I want to give back to my family the 15 years I lost.”
Hivi karibuni Marekani iliahidi kuendelea na mpango wake wa kuwahamisha wafungwa waliopo katika gereza la Guantanamo Bay kitendo ambacho kimekuwa kikipingwa vikali na Rais mteule wa nchi hiyo, Donald Trump.

ANGALIA BRAND NEW *VIDEO* YA JAGUAR FT EL – WARRIOR


ZILIZOSOMWA ZAIDI