Monday, November 30, 2015

MAJIBU YA NEYMAR KUHUSU KUSAJILIWA NA REAL MADRID

Barcelona-v-AS-Roma-Pre-Season-FriendlyNeymar
Baada ya kipigo cha goli 4 kwa bila kutoka kwa wapinzani wao Barcelona, habari za chini chini zilianza kusambaa kuwa Real Madrid inataka kuweka dau kwa staa wa Barcelona, Neymar.
Tetesi hizo zilidokeza kuwa rais wa Real Madrid, Florentino Perez alikuwa tayari kumuwekea mezani Neymar kitita cha Euro Milioni 190 ili kupata saini ya nyota huyo.
Baada ya tetesi hizo mtandao wa Espnfc umeripoti kuwa Neymar amesema hayupo tayari kujiunga na Real Madrid na jambo hilo halina nafasi kwake hasa baada ya kuwepo na habari kuwa mchezaji huyo anapewa mkataba mpya.
Aidha wakati wa kipindi cha joto Manchester United ilionesha kuhitaji huduma ya mchezaji huyo ambapo taarifa zinasema ofa hiyo anaweza ipokea kama ikiwa nzuri lakini kwenda Real Madrid haiwezekani.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI