Monday, March 30, 2015

15 MBARONI KWA NJAMA ZA KUTAKA KUMTOROSHA MCHUNGAJI GWAJIMA

KUJARIBU KUMTOROSHA MCHUNGAJI GWAJIMA KUTOKA HOSP. YA TMJ MIKOCHENI.
Mtoa taarifa ASP Pamphil Mholery OCS Kawe akiwa ni ofisa wa zamu mkoa Kinondoni,trehe 29.3.2015 majira ya 0300hrs alipata taarifa kutoka vyanzo vya taarifa kwamba kuna njama za kumtorosha mtuhumiwa.
Akiongozana na makachero majira ya 03:30hrs walifika eneo hilo na kukuta kweli kuna hali sio ya kawaida kwa kuwepo kundi la watu kwa usiku ule.
Wakawakamata watuhumiwa 15 na mmoja wao aitwae Ekomia Diagare alikutwa na begi ambalo lilikutwa na vitu vifuatavyo alivyokuwa akipelekewa Gwajima.

1.Silaha pisto Bereta no CAT 5802 ikiwa na risasi 3.

2.Risasi 17 za shortgun.

3.Vitabu check viwili

4.Passport ya kusafiria yenye jina Gwajima Mathias Joseph no AB544809.

5.Kitabu cha Equity Bank in check.

6.Document mbali mbali za kampuni ya Puma.

7.Charger ya simu na tablets

8.Suruali mbili,makoti mawili,singlend moja,socks pea mbili na boxer moja.
Watuhumiwa wote wako police Oyster kwa mahojiano.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI