Friday, October 30, 2015

LOUIS VAN GAAL AJIBU MASHAMBULIZI YA PAUL SCHOLES

Louis van Gaal amjibu Paul Scholes
Louis van Gaal amjibu Paul Scholes
Louis van Gaal amejibu mashambulizi kutoka kwa Paul Scholes kwamba Manchester United ni butu, kwa kusema: “Fimbo na mawe zitaumiza mifupa yangu lakini majina hayataniumiza!”
Gwiji wa Old Trafford Scholes amelalamika kuhusu “ukosefu wa kujituma na ubunifu” akidai kwamba asingependa kuchezea kikosi cha United cha sasa ambacho mechi zake mbili za mwisho zilimalizika bila magoli.
Van Gaal amesema atafanya kila awezalo kuipa mafanikio Manchester United
Van Gaal amesema atafanya kila awezalo kuipa mafanikio Manchester United
Van Gaal alisistiza kwamba timu yake huwa inajituma na kuburudisha, na kumshutumu Scholes kwa kutoa maoni kwa sababu analipwa na chombo cha habari.
Man U itavaana Crystal Palace siku ya Jumamosi
Man U itavaana Crystal Palace siku ya Jumamosi
Mholanzi alisema: “Scholes hana majukumu, hivyo anaweza kusema lolote. Kwanini anajisemea lolote? Hii ni kwa ajili ya klabu au kwa manufaa yake mwenyewe?
Paul Scholes amekikosoa kikosi cha Louis van Gaal
Paul Scholes amekikosoa kikosi cha Louis van Gaal
“Siwezi kujitetea mwenyewe kwa sababu siwezi kijitetea, kwa sababu ni gwiji na kwa sababu ana sauti kubwa, naisikia. Nafikiri unapokuwa gwiji, unapaswa kuzungumza na kocha au rafiki yake, Ryan Giggs, au Ed Woodward, lakini sio namna hi, kwa sababu atalipwa na BBC au Sky.
Louis van Gaal akiwa na msaidizi wake Ryan Giggs
Louis van Gaal akiwa na msaidizi wake Ryan Giggs
“Una muonekano wako. Daima natumia muonekano wa Uholanzi, lakini una muonekano mzuri ila fimbo na mawe zinaweza kunivunja mifupa yangu, lakini sio majina ya watu. Muonekano mzuri. Unaelewa maana yake?.
Louis van Gaal amesema hawezi kujitetea kwa maoni aliyotoa Paul Scholes
Louis van Gaal amesema hawezi kujitetea kwa maoni aliyotoa Paul Scholes
“Scholes akitaka niondoke, naondoka. Lakini sio jukumu lake, yeye sio Glazers au Ed Woodward.
“Najua lini tutapoteza kupoteza na kupoteza, nitakwisha, lakini nitafanya kila niwezalo kwenye hii klabu, kama nilivyosema, hii klabu sio ya kawaida.”

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI