Friday, October 30, 2015

CHINA YAFUTA SHERIA YA WANANDOA KUZAA MTOTO MMOJA, *SASA RUKSA WATOTO WAWILI*

CHINA yafuta sheria ya wanandoa kuzaa mtoto mmoja.
Hatimaye China kupitia shirika la habari nchini humo la Xinhua imeamua kufuta sheria iliyodumu kwa miongo mingi iliyokuwa ikizitaka familia za nchi hiyo kutokuzaa mtoto zaidi ya mmoja ‘one-child policy’.
Ambapo kwasasa wanandoa wameruhusiwa kuzaa watoto wawili ili kupunguza athari zinazoletwa na sheria ya mwaka 1979 ikiwa ni pamoja na kuzuia ongezeko la watoto milioni 400 na ongezeko kubwa la idadi ya watu wenye umri mkubwa wanaozidi idadi ya vijana nchini humo.
Hapo awali wanandoa waliokiuka sheria hiyo walipewa adhabu mbalimbali kama kulazimishwa kutoa mimba, kutozwa faini, na kufukuzwa kazi.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI