Wednesday, November 26, 2014

AJABU..!! MTOTO AZALIWA NA MIGUU MINNE NA MIKONO MINNE... AITWA "MUNGU MVULANA"

IMETOKEA nchini India baada ya mama mmoja kujifungua mtoto mwenye miguu minne na mikono minne huku akipokelewa na wenyeji kwa furaha kubwa na kuitwa ‘Mungu Mvulana’ 
Mtoto huyo amepewa jina la ‘Mungu Mvulana‘ kwa kuwa kuzaliwa na viungo kama hivyo si jambo la kawaida na huchukuliwa kama mfano wa Mungu kwa jamii za kihindu na watu walisafiri kutoka kona mbalimbali za nchi hiyo kwenda kumshuhudia mtoto huyo wa maajabu. 
Katika mji wa Kaskazini mwa nchi hiyo watu walijazana nje ya eneo la Hospitali hiyo wakiwa na hamu ya kutaka kumwona mtoto ambaye ana maana kubwa kwa jamii za nchini humo na wenyeji wa huko wana amini ataleta baraka katika jamii zao. 
Mamia ya watu walikua wamejaza nje ya Hospitali hiyo wakiimba na kusali lakini hawakuweza kufanikiwa kumwona kutokana na wingi wao huku Polisi wakitumia nguvu ya ziada kuwazuia. 
Baadhi ya watu walidiriki kusema ujio wa mtoto uyo ni dalili za mwisho wa dunia kutokana na jinsi baadhi ya jamii nchini humo zinavyoamini, Watalaam wa mambo ya uzazi walisema kuzaliwa mtoto huyo akiwa katika hali hiyo ilikua na dalili ya kuzaliwa watoto mapacha ambao kitaalam wanaitwa Parasitic twins lakini haikuwezekana na kudai ni mipango ya Mungu. 
Familia ya mtoto huyo imejawa na furaha kwa ongezeko la mwanafamilia mwingine na wanamuona mtoto huyo kama Mungu, mtoto wa kiume wa familia ya Wahindu,Brahma ambaye anatambulika kwa kuwa na miguu na mikono minne.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI