Sunday, October 28, 2012

SJMC NIGHT ILIVYOKOSHA NYOYO ZA WENGI.

vvvvKufahamu mazingira yanayokuzunguka huwa ni jambo jema sana kwa binadamu kwani humpa mwanadamu kujiamini kwa kile anachokifanya katika mazingira aliyopo.

Kufahamiana na watu aliowakuta katika mazingira hayo mageni pia huleta faraja na amani kwani hupata kujua historia mbalimbali za eneo hilo; watu, viumbe au hata vitu ambavyo vimeshawahi kuishi katika eneo hilo, na vinavyoendelea kuishi.

Vilevile moja kati ya vitu muhimu duniani ambavyo binadamu anapaswa kuwa navyo ni pamoja na kupata muda wa kurefresh na kuanza upya, kwani hata kiafya hupunguza msongo wa mawazo na kurejesha hali mpya katika mfumo mzima wa ufahamu na kupelekea ufanisi kuongezeka na afya ya akili kuimarika.

Kwa kulitambua hilo Serikali ya wanafunzi DARUSO-SJMC iliona ni vyema kuaandaa  hafla fupi ya kuwakaribisha wanafunzi wa certificate na mwaka wa kwanza ambao wao ni wageni katika mazingira haya kujumuika na wenzao wanaoendelea (continuous) kufurahia ujio wao hapa chuo na kufurahia kukutana na vijana wenyeji wenye kuwapenda wageni wao.

Kulikuwa na matukio mengi ambayo kiukweli ukifuatilia katika mfululizo hapa chini utagundua kuwa tukio hili lilikuwa ni maalumu kwa freshers na wenyeji wao kula bata!!! KARIBU UJIONEE...
Hafla hiyo ilianzwa kwa wadau wote kushiriki katika michezo.
Haya sasa wenye. 1, 2, 3 twendeeeeeh!!!
Vutaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!! jamani wewe usiachieeee!!!!!!
Chezea sisi wewe!!! Sisi ndio washindi, Hureeeeeh!!!!!!!!!!!
Haya sasa nani kidume!!!! twendeee vutaaaaaaaaaa!!!!!!!!
Bravooooo!!! Sam Mwalongo, Riziki Mashaka, Denis, Yasin mpooooo!!!!!?
Ngoja tuingie ukumbini sasa!!!
Tumetokelezea eeeeeh!!!!!!!? 







Ndipo baada ya michezo hiyo kamati teule ya shughuli hiyo, ikatambulishwa!!!

Mgeni rasmi mkuu wa shule kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa  Umma (SJMC) Dkt. Herbert Makoye akiwa na M/kiti wa Serikali ya wanafunzi DARUSO-SJMC Bw. Musa Ngwegwe, wakitazama shughuli inavyokwenda.
Mgeni rasmi mkuu wa shule kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa  Umma (SJMC) Dkt. Herbert Makoye akitoa nasaha kwa wanafunzi wa SJMC pamoja na wageni waalikwa waliokuwapo ukumbini hapo.


Baadhi ya wanafunzi na wageni waalikwa wakiwa bize kushudia shoo ya vijana matata (katika picha inayofuata)

Ebwana eeeh!! hawa kinadada balaa, usiwaone ukadhani wazembe. kwenye mguu upande wako fiti kalikiti.

Hii ni ME COLLECTION: Mamodo wamepozi katika foto ya pamoja huku wakiwa wametinga nguo bomba kutoka ME COLLECTION inayosimamiwa na mwanadada Dorcas Francis

Warembo wakiwa wametokelezea, wakiongozwa na mama Nice Lucas Siema (alievaa nguo ya madoamadoa) wakichabo mpango mzima wa shoo pale Girrafe Ocean View Hotel!

Warembo wa mwaka wa kwanza wakiwa wametokelezea kwa sana!!! safi sana.

Kwa wageni waalikwa nao ilikuwa ni shangwe kwani waliyazoea mazingira fasta na kula 'monde' kama kawa


Boy: Hey ujue umependeza na mimi nimepe so kama vipi tutacheza wote mziki eeh!
Girl: Mmmh!!!





Anonymus: ''Oya nani anaelewa ratiba inayofuatia???


Menu ilikaa poa balaa


Wosia kidogo kutoka kwa baba, Mwalimu Isa Mbura it was great having you sir.

Mziki ukafunguliwa bwana, kilichoendelea nadhani unaona picha hapo chini.
Kitu na boksi!
Freestyle sasa! Mc BRAVO akishusha mambo!
  (Picha zote na Hilali Ruhundwa 'PHD')

1 comments:

  1. Kaka nimekumbuka mbali sna hyo issue dah ... Riziki hapa

    ReplyDelete

ZILIZOSOMWA ZAIDI