Sunday, October 28, 2012

MAMA WA MTOTO ALIYEKOJOLEA MSAAFU AOMBA RADHI.



HATIMAYE mama wa mtoto aliyekojolea msaafu na baadae kuzua gumzo ndani ya waumini wa dini ya kiislam na wakristo ambalo limepelekea mali nyingi ikiwemo kuteketezwa kwa makanisa huko Mbagala jijini Dar es salaam, watu kupoteza uhai, na wengine wakiwa hospitalini bado wakijiuguza majeraha.

Inaripotiwa kuwa mama huyo Bi. Teresia Josephat siku ya jumamosi katika mahojiano na mwandishi wa gazeti amesema kuwa hajawahi tegemea kama kitendo hicho kingefanywa na mwanae Emmanuel Josephat (14) kwani alimkuza katika malezi na maadili mema tu.

Mda mrefu kidogo umepita, katika mabishano ya rika kati ya kijana huyo na wenzake, ndipo ikafikia kijana huyo kukidhihaki kitabu kitukufu cha kuruani  kwa madai kwamba angelifanywa hivyo angeweza kugeuka mnyam

Mtandao huu UNAPINGA na KULAANI kitendo cha mtu wa dini fulani kumdharau au kumuona hana haki mtu wa dini nyingine, wote tunamwabudu Mungu mmoja hivyo yatupasa kujitakasa kwa kutodharauliana kiimani.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI