Monday, October 31, 2016

DARASSA ADAI KUJA NA COLLABO NA CHRISTIAN BELLA

Rapper Darassa amefunguka kuwa muda si mrefu atakuja na collabo yake na Christian Bella.
Akiongea na kipindi cha Clouds Top 20 cha Clouds FM, Darassa amesema kuwa amefurahi kusikia kuwa Bella anamkubali sana kwa hiyo mashabiki watarajie kazi yao ya pamoja.
“Jana [Jumamosi] tulikuwa tumekaa sehemu nikasikia mtu anasema kuwa Christian Bella ananikubali sana, hata mimi ni shabiki wake mkubwa. Tumepanga kufanya collabo, mashabiki wasubirie kitu kikubwa,” amesema Darassa.

Kwa sasa Darassa ni mmoja kati ya rapper wa kizazi kipya ambao kazi zao zinafanya vizuri kwenye Redio na TV mbalimbali.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI