Thursday, November 29, 2012

WILDAF NA SIKU 16 DHIDI YA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA TZ

Ni katika maandalizi ya Kipindi cha JAHARA kinachorushwa kila siku za wiki kuanzia Jumatatu mpaka Jumamosi, Pichani ni Mtangazaji wa kipindi hicho Bw Spencer Lameck na Bi. Anna Kulaya ambaye ni Afisa Mwandamizi katika shirika ambalo si la Kiserikali WILDAF.
Bi. Ana Kulaya akiongea juu ya shirika la WILDAF lakini zaidi akieleza jinsi shirika hilo linavyofanya kazi, lakini pia akapata fursa ya kuielezea Kampeni ya SIKU 16 DHIDI YA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA TANZANIA kampeni ambayo imefanyika hivi karibuni lakini pia hufanyika kila mwaka mnamo tarehe 25 Novemba kupinga vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto.
Bi. Jackline Waya,pia ni Afisa mmojawapo katika shirika la WILDAF ambapo akapata fursa ya kuelezea malengo ya kampeni hiyo na zaidi malengo ya Shirika hilo.

USIKOSE KUANGALIA KIPINDI HIKI CHA JAHARA IFIKAPO SIKU YA IJUMAA SAA MOJA MPAKA SAA MOJA NA NUSU ASUBUHI.

KAMA UNA JAMBO AMBALO NI LA MANUFAA KWA UMMA WA WATANZANIA NA UNGEPENDA UMMA HUO ULIPATE, BASI KATIKA KIPINDI HIKI UTAPA FURSA HIYO, WASILIANA NA MTAYARISHAJI NA MHARIRI WA KIPINDI HIKI KWA NAMBA ZIFUATAZO: +255 652 294 780, +255 719 583 949

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI