Thursday, November 29, 2012

WAOMBOLEZAJI: ''SAFARI NJEMA SHARO WETU''

ULIMWENGU WA HABARI KATIKA PICHA
Jeneza  lenye  mwili wa Sharo Milionea  likitolewa 


Wananchi  wakiwa na huzuni wakati  mwili wa Sharo Milionea  ukitolewa 



Umati  wa  waombolezaji  wakiwa nyumbani kwa Sharo Milionea 

Shekh akiombea  mwili  wa jeneza  leye mwili wa Sharo Milionea


Waumini wa dini ya kiislamu  mkoani Tanga  wakiufanyia  dua za mwisho mwili wa Sharo Milionea 

 Mwili wa Marehemu Sharo Milionea ukiswaliwa hapo jana kabla ya kupelekwa kwenye nyumba yake ya milele 
Hapa  ndipo  mwili wa Sharo Milionea  ulipohifadhiwa
 Rafiki mkubwa wa marehemu Sharo Milionea, Mzee Majuto akiwa ameshikwa mkono wakielekea kwenye mazishi, Muheza mkoani Tanga.

MAMIA ya wakazi  wa mkoa  wa Tanga pamoja na  wasanii wa  kundi la Bongo Movie wameshiriki kikamilifu katika mazishi ya msanii Sharo Milionea yaliyofanyika  wilayani Muheza mkoani Tanga eneo la umbali wa takribani kilometa 2 kutoka nyumbani  kwa msanii  huyo.

Imedaiwa kuwa umati  mkubwa wa wananchi wamejitokeza kwa wingi  kuuaga mwili  wa msanii  huyo huku  baadhi  wakigombea  kuaga mwili  huo, kitendo kilichopelekea upotevu wa amani kwa muda.

Hata  hivyo  vurugu hizo zilidaiwa kutokea  wakati  wa  kuuaga mwili ambapo  kila mmoja aliyejitokeza eneo hilo alitaka  kuugusa  mwili  wa Sharo Milionea .

Miongoni  mwa  viongozi  wa  vyama  vya  siasa  waliofika  ni pamoja na  Nappe Nnauye, Mukama, huku Miongoni  mwa  wasanii wa Bongo Movie waliofika hapo ni pamoja na Vicent Kigosi 'Ray', Kitale pamoja na wengine wengi.

Mwili  huo  umezikwa  eneo la umbali  wa kilomita  2  kutoka  nyumbani kwao marehemu. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU SHARO, PEMA PEPONI. AMIN!

Habari kwa hisani ya mtandao wa francis godwin

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI