Friday, May 30, 2014

KAMATI TENDAJI YA TAIFA YA MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII TASAF, YAZURU KIBAHA, PWANI.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Ladislaus Mwamanga (aliyesimama)akitoa ufafanuzi juuya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kwa walengwa wa Mpango huo(hawapo pichani).
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Tatu Seleman(mwenye miwani) akiangalia moja ya mikeka iliyosukwa na walengwa wa Mpango waKunusuru Kaya masikini,PSSN, katika kijiji cha Vikuge kama njia mojawapo ya kukuzakipato cha wananchi.
Walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji cha Vikuge wilaya yaKibaha mkoani Pwani wakiwa katika mkutano uliohudhuriwa pia na wajumbe wa kamatitendaji ya TASAF (hawapo pichani) iliyotembelea kijiji hicho kukagua shughuli za Mpangohuo zinavyoendelea.
Karibu wageni hivi ndivyo anavyoelekea kusema Mkuu wa mkoa wa Pwani MwantumuMahiza(aliyeko mbele ya wajumbe) wakati alipowakaribisha wajumbe wa kamati tendaji yaTASAF iliyomtembelea ofisini kwake kabla ya kutembelea vijiji vya Vikuge na Misufinikukutana na walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masikini,PSSN.
Kaimu mwenyekiti wa kamati tendaji ya TASAF Abbas Kandoro (katikati) akisisitizajambo mbele ya Mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza (aliyevaa kilemba) wakatiwajumbe wa kamati hiyo walipomtembelea mkuu huyo wa mkoa wa Pwani ofisini kwakekabla ya kutembelea vijiji vya Vikuge na Misufini katika wilaya ya Kibaha kukaguwashughuli za walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya masikini unaoratibiwa na TASAF,kushoto kwa Kandoro ni Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga
Kamati Tendaji ya Taifa ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF, yazuru Kibaha, Pwani.
Wajumbe wa kamati tendaji ya Taifa ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii,TASAF wamefanyaziara katika vijiji vya Vikuge na Misufini katika wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani kuonanamna walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masikini na zinazoishi katika mazingirahatarishi,PSSN, wanavyonufaika na mpango huo.
Kabla ya kutembelea vijiji hivyo wajumbe wa kamati hiyo walikutana na mkuu wa mkoawa Pwani Mwantumu Mahiza ambaye alionyesha kuridhishwa kwake na namna TASAFinavyochangia jitihada za wakazi wa mkoa wake kupambana na umasikini.
Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani amesema mabadiliko ya kujivunia yameanza kuonekanakatika nyanja za elimu, afya,makazi na hata uchumi hususani kwenye maeneo ambayoTASAF inatekeleza mpango huo wa PSSN.
Katika vijiji vya Vikuga na Misufini walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masikiniwamebainisha kuwa mpango huo umesisimua kwa kiwango kikubwa shughuli zamaendeleo miongoni mwao huku wakibainisha kuwa hata uwezo wa kuwahudumia watotokwenda shule na kupata huduma za afya umeongezeka.
Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo tendaji ya TASAF, ABBAS KANDORO akizungumzana walengwa wa mpango huo amewataka kutobweteka na mafanikio waliyoanzakuyapata kutokana na mpango huo wa TASAF bali waendelee kuongeza juhudi katikauzalishaji mali ili hatimaye waweze kujikwamua kutoka katika dimbwi la umasikini.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga amebainisha kuwa taratibuzinakamishwa ili hatimaye watoto walioko katika kaya masikini ambao wamefaulukujiunga na masomo ya sekondari waweze kuhudumiwa kupitia Mpango wa kunusurukaya masikini kuanzia mwezi Julai mwaka huu.
Mwamanga amesema hali hiyo imetokana na Mfuko kubaini kuwa idadi kubwa ya kayamasikini zilizoingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini watoto waowameitikia wito wa kuhudhuria masomo kama mojawapo ya masharti na hivyo wengiwao kufaulu kujiunga na masomo ya sekondari lakini changamoto iliyoko ni uwezomdogo wa kaya husika kuwasomesha watoto hao katika ngazi ya sekondari.
Wajumbe wa kamati tendaji ya TASAF chini ya mwenyekiti wake mpya FlorensTuruka ambaye pia ni katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu leo na keshowanahudhuria kikao cha bodi hiyo jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI