Saturday, November 1, 2014

WIZ KHALIFA AZUNGUMZIA SABABU ZA KUACHA KUVUTA BANGI, KWA SASA ANAITWA 'WEEDHEAD'.

KATIKA Interview aliyofanyiwa Wiz Khalifa hivi karibuni anazungumzia kubadilisha mtazamo wa mashabiki na watu ju yake, Wiz anasema anampango wa kubadilisha muonekano wake ili uwe na mzuto wa kibiashara zaidi.
Wiz anasema "Sitaki tena watu wahusishe muziki wangu na marijuana" kama unakumbuka mixtape za kwanza za Wiz Khalifa kama ya mwaka 2010 Kush & Orange Juice,

Wiz anaendelea kusema "sipendi kuitwa kicha cha bangi "weed head" na nataka nifanye kazi bila kuandamwa na mtazamo huo wa kibangi bangi. Waigizaji wakubwa kwenye filamu hawana muonekano wa kibangi bangi sasa kwanini mimi niendekeze hii tabia, nitaacha kuimba kuhusu bangi na nampango wa kuacha kuvuta kabisa, Inaharibu muonekano wangu na mtazamo wa kazi zangu kwa watu" . 

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI