Friday, January 6, 2017

RIYAD MAHREZ ATUMA UJUMBE KWA MASHABIKI BAADA YA KUSHINDA TUZO

NI furaha kwa kila mtu pindi mchango wake unapoonekana na kupewa zawadi – ndicho kilichomtokea Riyad Mahrez usiku wa Alhamisi hii baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa kuwabwaga washiriki wengine akiwemo Pierre-Emerick Aubameyang na Sadio Mane.
Mahrez ambaye ni mchezaji wa Algeria amewashukuru mashabiki wote duniani kutokana na kuwa na msimu mzuri kwa mwaka jana na kufanikiwa kuisaidia timu yake ya Leicester City kushinda taji la ligi kuu ya Uingereza.
Kupiti kwenye mitandao yake ya kijamii, mchezaji huyo ameandika, “African ballon d’or … I thank everyone who supporte me around Africa and around the world .”
Hii ni tuzo ya tatu kubwa kushinda kwa mchezaji huyu baada ya ile ya ‘Mchezaji bora wa mwaka ya chama cha wachezaji soka ya kulipwa Uingereza (PFA) na ‘BBC African Player of the Year’.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI