Saturday, October 29, 2016

DUMA WA SIRI YA MTUNGI KUACHIA ‘CHUN’TAMA’ AKIWA NA MASTAA KIBAO

Msanii wa filamu Daudi Michael Tairo, anayefahamika zaidi kwa jina la Duma ndani ya tamthilia ya Siri ya Mtungi, amejipanga kuachia filamu yake mpya iitwayo ‘Chun’tama’.
Mwigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa filamu hiyo itakuwa inazungumzia maisha halisi wa watanzania pamoja na masuala ya uchawi.
“Baada ya kufanya vizuri katika filamu yangu ya ‘Mchongo Sio’ nikaona nisikae kimya sana. Kwahiyo nimeamua kuachia filamu mpya inaitwa Chun’tama. kwenye filamu hiyo kuna mastaa kibao, Grace Mapunda, Chuchu Hans, Hashim Kambi, Barafu Suleiman na wengineo kibao. Na filamu inamatukio mengi pamoja na mambo yakichawi ndani yake,”

Pia mwigizaji huyo amesema hataki kuwaangusha mashabiki wake wa filamu ndiyo maana hataki kukaa muda mrefu bila kuachia filamu mpya.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI