Saturday, March 5, 2016

KOCHA MKUU WA MBEYA CITY KINNAH PHIRI ATAJA WACHEZAJI 18 WATAKAO CHUANA NA SIMBA FC

Kocha Mkuu wa Mbeya City Fc, Kinnah Phiri ametangaza majina ya nyota 18 watakaoivaa Simba Sports Club kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliopangwa kuchezwa jumapili hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Phiri ameuambia mtandao huu kuwa anatua jijini Dar na kikosi cha nyota hao ambao aliwaandaa maalumu kwa mchezo huo wa mwishoni mwa juma akiwa na imani kubwa kuwa wataiwezesha City kuibuka na ushindi kutokana na ‘kuiva’ vizuri kimazoezi na mafunzo waliyoyapata katika wiki nzima ya maandalizi kupitia mifumo mbalimbali aliyokuwa akiifundisha .

“Nina imani nao,wamefanya vizuri sana kwenye mazoezi ya wiki hii, sina shaka na wao kutupatia matokeo kwa sababu wako sawa tayari kwa mchezo,tutacheza kwenye mfumo mpya ambao haujawahi kuonekana tukicheza, hii ni kwa sababu tumedhamiria kupata ushindi kama ambavyo timu imekuwa ikifanya kila inapokutana na Simba”, alisema.

Miongoni mwa nyota walio kwenye orodha ya kuivaa Simba siku hiyo ya jumapili ni pamoja na beki wa kushotoHassan Mwasapili, mlinda lango Haningtony Kalyesubula pia wamo Temi Felix, Haruna Shamte,Yohana Moriss,Kenny Ally,Geoffrey Mlawa,Issa Nelson na wakali wengine 10 ambao wamepewa majukumu kadhaa kuhakikisha City inaandikisha pointi tatu muhimu mbele ya timu hiyo ya Msimbazi.

Huu utakuwa ni mchezo wa sita kwa timu hizi kukutana katika michuano hii ya ligi kuu ya vodacom huku City ikifanikiwa kushinda mara mara mbili sare mbili na Simba ikishinda mara moja katika michezo mitano iliyozikatanisha timu hizi hapo awali.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI