Tuesday, January 26, 2016

WEMA SEPETU KUJIFUNGUA MWEZI AUGUST

Malkia wa filamu, Wema Sepetu anatarajia kujifungua mwezi August 2016, kwa mujibu wa mpenzi wake Idris Sultan.
Akizungumza katika kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM Jumanne hii, Idris alisema mpenzi wake huyo anatarajia kupata mtoto baada ya miezi 6 au 7 hali ambayo imetafsiriwa na wadau wa mambo kuwa huenda mwanadada huyo akawa na mimba ya miezi 3 au 2.
“Yes very soon natarajia kupata mtoto kama miezi 6 au 7 ijayo,” alisema Idris. Pia Idris alisema bado hajatambua jinsia ya mtoto anayetarajia kujifungua mpenzi wake.
“No hatujui mwenzangu anataka surprise. Mimi nataka kujua kabla kwahiyo bado hatujafikia muafaka, naogopa nisije nikawa nanunua vigauni akaja Wa kiume bure,” alisema.
Aliongeza, “Huwezi kuwazuia watu kuongea, waache waongee maana sometimes watu ni wagumu kupokea changes lakini siku zinavyoenda naamini wataelewa tu.”
Pia Idris alisema wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI