Sunday, June 28, 2015

ZIARA YA KINANA KATIKA JIMBO LA NYAMAGANA

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi kutoka wilaya ya Nyamagana wanaounda makundi ya Machinga,Bodaboda, na Mama Lishe kwenye uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na makundi ya Mama Lishe ,Machinga na Boda boda katika kikao kilichofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
 Baadhi ya Mama lishe waliohudhulia kikao na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Nyamagana kwenye ukumbi wa BOT mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi na taarifa ya kazi za Chama.
 Daraja la zamani la Isegeng’e lililopo kata ya Mahina.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria kufunguliwa kwa daraja  jipya la Isegeng’e, kata ya Mahina wilaya ya Nyamagana.
 Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Mhe.Stanslaus Mabula akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa CCM Igoma.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Igoma wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Igoma na kuwaambia kuwa wachague viongozi wanaojali watu ili kusaidia kuleta maendeleo kwa haraka.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimia wakazi wa kata ya Buhongwa wakati wa ufunguzi wa jengo la kitega uchumi la CCM Buhongwa.
 Wakazi wa Buhongwa wakifurahia mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM wakati wa sherehe za ufunguzi wa kitega uchumi cha CCM kata ya Buhongwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Buhongwa na kuupongeza Uongozi wa kata ya Buhongwa kwa kujenga kitega uchumi hicho kushirikiana na muwekezaji wa ndani.
 Umati wa wakazi wa kata ya Buhongwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Vijana wa Nyegezi wakimpokea katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa shangwe ya kipekee.
 Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Mhe. Stanslaus Mabula akizungumza wakati wa mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM na Vijana wa Boda boda wa Nyegezi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu Vijana wa Boda Boda wa Nyegezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Vijana wa Boda Boda wa Nyegezi ambapo aliwaambia ni vyema kuchagua viongozi watakaosaidia Vijana katika maendeleo yao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipandisha bendera wakati wa uzinduzi wa Shina la UVCCM Bungeni,Nyegezi wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza. (Picha zote na Adam Mzee)

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI