Friday, March 20, 2015

MHUDUMU WA BAR AFIKISHWA POLISI BAADA YA KUDAGANYA JINSIA YA MWANAMKE KUMBE NI DUME

UGUMU wa maisha unaongeza ubunifu, ubunifu mwingine unakuweka pabaya.. huu wa huyu jamaa
sidhani kama tunaweza kuuita ni ubunifu ila jamaa aliamua tu atumie njia hii ili apate tu njia ya kupata mkate wa siku.

Mmiliki wa Bar ya Siaya, Kenya alimshtukia jinsia ya mmoja ya wahudumu wake wa Bar kwamba jinsia yake
sio ya kike.. Akatoa taarifa Polisi kuhusu mhudumu huyo, walipokuja kumpekua jamaa alijitetea kwamba ana jinsia mbili.

Jamaa huyo anaitwa Michael Obiero alikamatwa baada ya kufanya kazi kwa siku mbili kwenye Bar hiyo
akijitambulisha kwa jina la Brenda na pia alikuwa akilala chumba kimoja na wahudumu wengine wa kike

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI