Friday, December 7, 2012

WANAHABARI WAMJULIA HALI MWANDISHI SHAABAN MATUTU


 Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu akiongea na waandishi wa habari na wadau mbalimbali waliofika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam baada ya kutolewa risasi kifuani aliyopigwa na Polisi nyumbani kwake Tegeta.
 Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu akisalimiwa na wadau na waandishi mbalimbali waliofika kumjulia hali akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam baada ya kutolewa risasi kifuani aliyopigwa na Polisi nyumbani kwake Tegeta.
Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu akionyesha sehemu aliyojeruhiwa na risasi baada ya kujuliwa hali na waandishi wa habari katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam baada ya kutolewa risasi kifuani aliyopigwa na Polisi nyumbani kwake Tegeta.
(Picha zote na Francis Dande)

Kamanda Suleiman Kova akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Ambapo jana tu, kamanda Suleiman Kova amesema kuwa uchunguzi juu ya jambo hili unafanya na jeshi la polisi, na kuwachukulia hatua wote watakao kuwa wamehusika na tukio hili kwa namna moja ama nyingine.

‘’Yeyote Yule ambaye ataonekana kuwa amehusika kwa namna moja ama nyingine atachukuliwa hatua’’ Hayo ni maneno aliyoyasema kamanda Suleiman Kova katika mkutano na waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa kamanda Suleiman Kova askari mmoja ameshakamatwa akihusishwa na tukio la mauaji ya marehemu John Paul ambaye inasemekana alijeruhiwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya wananchi waliokuwa wakipinga kukamatwa magari yaliyopaki sehemu isiyoruhusiwa eneo la Tegeta kwa ndevu jijini Dar es salaam wiki iliyopita.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI