Friday, November 30, 2012

AIRTEL YAMUANDALIA PARTY AY KUMPONGEZA KWA KUPATA USHINDI

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo flava)  na Balozi wa Airttel Tanzania, Ambwene Yessaya 'AY' akiwa ameshika tuzo hiyo aliyozawadiwa hivi karibuni katika mashindano ya Chanel-O huko Afrika Kusini.
Afisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde na Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo flava) kwa pamoja wakionyesha tuzo ya  Channel O  aliyoipata Mwanamuzi huyo nchini Afrika Kusini. Tukio hilo limefanyika leo wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo Airtel imempongeza AY kwa ushindi alioupata pamoja na kumwandalia sherehe ya kumpongeza itakayofanyika leo usiku nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam 
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo flava)  na Balozi wa Ambwene Yessaya 'AY' akiwashukuru watanzania kwa kumpigia kura na kumwezesha kupata tuzo hiyo kulia ni Afisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde na kushoto ni  DJ wake Athur Baraka.
Afisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde akiongea wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo Airtel imempongeza AY balozi wake kwa kupata tuzo ya chanel O ya video bora, Katikati ni AY  akifatiwa na DJ wake Athur Baraka.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI