Tuesday, November 22, 2016

HANS VAN PLUIJM AKUTANA NA RUNGU LA TFF

KOCHA wa Yanga, Hans van Pluijm ambaye saivi amepata cheo na kuwa mkurugenzi wa Michezo wa klabu hiyo, amepigwa faini ya sh. 500,000 na kufungiwa mechi tatu baada ya Kamati ya Saa 72 ya TFF kukaa na kubaini ana makosa anadaiwa kuwazonga waamuzi na kuwatolea maneno ya kashfa.
Pia baada ya mechi kumalizika alikwenda kwenye chumba cha waamuzi na kuwatolea maneno ya kashfa. Adhabu hiyo ni kwa uzingativu wa Kanuni ya 40(1).
Klabu ya Yanga pia imepigwa faini ya sh. 500,000 baada ya washabiki wake kuwazonga waamuzi na kuwatolea maneno ya kashfa walipokuwa wakiingia vyumbani wakati wa mapumziko. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1).

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI