Saturday, October 29, 2016

NEW COUPLE IN TOWN: MPENZI MPYA WA LINAH MMMH!

Ule usemi wa Kiswahili unaosema ‘penzi ni kikohozi kulificha hauwezi’ unazidi kujidhihirisha kwa malkia wa muziki Linah Sanga baada ya kumweka wazi mpenzi wake mpya ikiwa miezi 6 toka adai hatoweka tena mahusiano yake wazi.
Linah akiwa na mpenzi wake
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Raha Jipe Mwenyewe’ mapema mwaka huu alidai kuweka wazi mahusiano yake ya mapenzi kunamwaribia muziki wake kutokana na mashabiki wake kupenda kufuatilia mambo yake ya ndani kuliko muziki wake.
Ijumaa hii muimbaji huyo ambaye pia aliwahi kutoka kimapenzi na Barakah The Prince ameamua kumweka wazi mpenzi wake mpya.
“Penzi sio kama nyanya itokayo sokoni, nipe penzi mwanana niliote ndotoni. I love u cheusi wangu @director_ghost #maramojamojasiyombaya #rahajipemwenyewe,” Linah aliandika istagram kupitia hiyo picha hapo juu.

Muimbaji huyo ni moja kati ya waimbaji wa kike ambao wanafanya vizuri katika tasnia ya muziki.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI