Sunday, September 27, 2015

MAGUFULI AZOMEWA JIJINI MBEYA.....WANANCHI WASEMA WANAMTAKA LOWASSA. *VIDEOZ*

Katika  hali  isiyo  ya  kawaida,Mgombea  Urais  kwa  tiketi  ya  CCM, Dr. John Magufuli  leo  alijikuta  katika  wakati  mgumu  baada  ya  kukutana  na zomea zomea  ya  kundi  la  vijana  waliovamia  msafara  wake  akiwa  njianI  kuelekea  Mbarali  na kuanza  kuimba wakidai  Lowassa  ndo  Rais  wao....Tazama  Video hii

Pamoja  na  kadhia  hiyo,Magufuli  alifanikiwa kufika  Mbarali  na  kuhutubia  maelfu  ya  wananchi  ambao  amewaahidi  kushughulikia  migogoro  yao  ya  muda  mrefu  ambayo  imekuwa  kete  ya  kuombea  kura  kwa  baadhi  ya  wanasiasa  wenye  uchu  wa  madaraka. Tazama Na Hii

Dr. Magufuli  leo  pia  amefanya  mikutano  kadhaa  ya  kampeni  mkoani  Iringa  ambako  alilazimika  kumalizia  viporo  hivyo vilivyokuwa  vimebaki  mkoani  humo. 
Wananchi kwa maelfu wakimsikiliza Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia huko Makambako mkoani Iringa ambako alipita leo kumalizia viporo vya mkoa huo kwenye kampeni zake.

Wagombea wa nafasi mbalimbali wa Mafinga wali-Magufulika mbele ya Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt. John Pombe Magufuli katika jimbo la Mafinga mkoani Iringa ambako alipita leo kumalizia viporo vya mkoa huo kwenye kampeni zake.
Mgombe ubunge jimbo la Mafinga Mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Cosato Chumi, aki-Magufuli-ka
Mgombea Ubunge Jimbo la Mufindi Kaskazini, Mahamudu Mgimwa akidhihirisha kuwa yupo fiti.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI