Tuesday, March 31, 2015

MFAHAMU YULE MRIMBWENDE WA KIJAPAN ALIYEDAIWA KUWA SI MJAPANI *PICHAZ*

Mrimbwende wa japan ameleta kizaazaa baada ya watu kuanza kuhoji Ujapan wake eti kwa kuwa kazaliwa na mama Mjapan na baba mwafrika.
Baba mwenyewe ni mwafrika kutoka Marekani.
Mrimbwende huyu ambaye pia amesomea nchini Marekani anazungumza Kijapan kama lugha yake ya kwanza na mama yake ni Mjapan  kikwelikweli.
Pamoja na ukweli kwamba alizaliwa na kulelewa Japan mrimbwende huyu Ariana Miyamoto  anaonekana katika macho ya wajapan kwamba si Mjapan wa kihivyo, lakini kisheria na hata kwa tafsiri ya nani ni mjapan hakuna shaka anaswihi.
Nchini japan watu wlaiochanganya damu wanaitwa "hafu", na ushindi wa Miyamoto kuwakilisha japan katika Miss Universe kumeleta mtafaruku mkubwa hasa katika vyombo vya habari kwamba inakuwaje hafu awasilishe japn kama Mjapan kamili.
Mdada huyo ambaye amejaliwa miguu ameleta taabu kiasi cha watu kuuliza katika vyombo vya habari kama ni sawa kwa hafu kuiwakilisha Japan.
Mrembo huyu anakuwa hafu wa kwanza kuwakilisha taifa hilo katika michuano ya urembo duniani Miss Universe.
Pamoja na mafanikio makubwa, ushindi wake haukuja kirahisi katika nchi ambayo haina mchanganyiko wa kutosha wa damu.
Akiwa na urefu wa futi sita akiwa katika viatu vya mchuchumio, binti huyu wa miaka 20 analazimika kujihami baada ya kudaiwa kwamba yeye si Mjapan hasa kwa kuwa baba yake ni mtu mweusi kutoka Arkansas, Marekani.



Miyamoto, amekulia Nagasaki, Japan, na pia alifika Marekani kwa ajili ya kujipatia elimu.
Kutokna na mchanganyiko na hasa kusomea Marekani baadhi ya wajapn wanaona kwamba yeye si Mjapan halisi na hafai kuwaikilisha nchi hiyo katika michuano ya urembo kama Mjapan.
Binti huyo alitumia  muda wake wa kwanza kutokea katika televisheni kuwaeleza waandishi wa habari kwamba japo anaoinekana kwa nje yeye sio mjapan lakini ndani yake yeye ana vitu vingi vinavyomuashiria kuwa yeye ni mjapan.
Katika mahojianoi na CNN alisema kwamba  amekuwa akipata taabu sana nchini japan kwani hata katika makuzi yake watu walikuwa wakimtenga, wakimvurumusha na hata kumtupoia uchafu kwa madai kwamba yeye si mjapan.

 
Kwa mujibu wa tafsri iliyofanywa na Washington Post, katika moja ya twita ilisema kuwa japo anawakilisha Japan katika shindano hilo sura yake inaonesha kwamba yeye si Mjapan hata kama unataka kujikomba.
Mwingine alisema, "Miss Universe Japan  ni... Nini?Huyu ni mtu wa aina gani?Sio Mjapan, sawa?"
Ingawa webu ya Kotaku ilipongeza ushindi wa Miyamoto na kusema ni dalili kwamba japan inabadilika japo kw ataratibu sana imesema kwamba wengi wa waliotoa maoni yaow alitaka mwakilishi ambaye ni Mjapan kwa kila kitu.
Hata hivyo si kila mtu anafikiria kinyume, wapo wengi waliounga mkono kufanikiwa kwake na mitandao ya jamii ilisema kinachojalishwa ni mapenzi kwa nchi wala si wajihi.
Na wengine wamesema kilio kwamba si Mjapan hasa ni shauri la kijinga na fikira za kizamani sana.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI