Saturday, January 31, 2015

HATIMAYE PROF. SOSPETER MUHONGO AKABIDHI OFISI KWA SIMBACHAWENE JIJINI DAR LEO *PICHAZ*

Waziri  mpya wa Nishati na Madini,George Simbachawene (kulia)
akikabidhiwa rasmi nyaraka za ofisi na Aliyekuwa Waziri wa Nishati na
Madini, Profesa Sospeter Muhongo, leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Waziri  mpya wa Nishati na Madini,George Simbachawene (kulia)
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati makabidhiano
ya ofisi na Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo, leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

ALIYEKUWA Waziri wa Nishati na Madini,Profesa Sospeter Muhongo amesema uadilifu unahitajika katika sekta ya Nishati na Madini pasiwepo na rushwa kwani hiyo ni kuweza kusaidia watanzania masikini wanaongalia sekta hiyo kwa maendeleo ya uchumi wao.

Muhongo ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akikakabidhi ofisi kwa Waziri  mpya wa Nishati na Madini,George Simbachawene,amesema lazima kuwepo na uzinagatiaji wa mikataba ili watanzania waweze kunufaika na rasilimali zao.

Muhongo amesema Simbachawene sio mtu wa tamaa siku zote alipokuwa Naibu wa Waziri wa Nishati na Madini walikuwa wakiambiana juu ya kuwatumikia watanzania wengi na sio mtu binafsi.

Amesema lazima tujenge uchumi imara kutokana na sekta hii ili watanzania waweze kukua kiuchumi kutokana na sekta ya madini inavyokua kwa kasi.

Muhongo amewataka waandishi kuelimisha watanzania kwa ajili ya ustawi wa taifa na sio mtu mmoja au ubinafis wa mtu.

Kwa upande wa Simbachawene amesema ataendeleza mazuri yaliyoachwa na mtangulizi wake kwa  kuweka uwazi kwa kila kitu kinachofanyika,kwani ofisi ya umma sio mali ya mtu.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI