Friday, November 28, 2014

MCHEZAJI WA CRICKET TOKA AUSTRALIA PHILLIP HUGHES AFARIKI DUNIA..! SOMA CHANZO!

MCHEZAJI wa cricket kutoka australia Phillip Hughes afariki duniana baada ya kupigwa shingoni na mpira  wa mchezo huo na kusabibishwa kutokwa na damu nyingi kichwani ilio sababisha kifo chake.
Hughes alikua akijiandaa kupiga mpira uliorushwa na timu pinzani kati ya mechi ya South Wales na South Australia siku ya jumanne baada ya mpira huo kumpiga upande wa kushoto wa shingo yake.
Phillip mwenye umbri wa miaka 25 anaechezea timu ya South Astralia  baada ya kupigwa na mpira huo alibaki  akisimama kwa mda mchache na baadaye alianguka chini na  kuzimia ambapo mapema jana alifariki dunia.
Daktari wa timu ya South Australia  Peter Brukner alieleza kua kupigwa kwake na mpira wa shingo na kutokwa na damu  nyingi kichwani ni tatizo la kushangaza maana ni nadra sana kutokea na kusababisha kifo cha mtu.
Kuna kesi 100 zilizowai kuripotiwa juu ya mchezo huu lakini hii ambayo ni adimu kutokea ni mara ya kwanza kuripotiwa.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI