Tuesday, October 21, 2014

MSANII LINAH ATHIBITISHA KUTOMPA 'MAMBOZ' MCHUMBA WAKE BAADA YA KUTIBUANA...! *PICHAZ*

MCHELE ulionyooka! Staa wa Bongo Fleva, mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Estelina Sanga ‘Linah’ na mchumba’ke, Nangari Kombo wanadaiwa kutibuana, kisa kikidaiwa ni maneno ya wanafiki yasiyokuwa na ukweli.
Staa wa Bongo Fleva, mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Estelina Sanga ‘Linah’
Habari za chini ya kapeti zilinyetisha kwamba mtiti kati ya wawili hao ulijiri juzikati baada ya Kombo kudaiwa kuanza kumtuhumu Linah kuwa anapokuwa kwenye ziara za matamasha kama Fiesta huwa anamsaliti na wanaume wengine.
 
Lina akiwa na mpenzi wake, Nangari Kombo.
Chanzo hicho kilidai kwamba, kufuatia madai hayo Kombo alimuanzishia Linah bonge la tafrani na kujikuta kila mmoja anachukua hamsini zake. Linah alipoulizwa kuhusu ishu hiyo alisema:
“Ni kweli kulitokea kutoelewana but (lakini) tumeyamaliza, tupo vizuri sana.”

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI