Wednesday, April 30, 2014

ELIMU KWA MADEREVA KUHUSU MABADILIKO YA NJIA ZA KATIKATI YA JIJI, MADEREVA KUWENI MAKINI KUSOMA ALAMA

 Askari wa Usalama Barabarani akitoa elimu ya mabadiliko ya njia za katikati ya Jiji la Dar es Salaam, kwa dereva wa gari dogo lenye namba za usajiri T 357 BZT, wakati likitaka kuelekea njia yenye alama inayozuia kupanda kutokana na mabadiliko ya njia ambayo yameanza rasmi kutumika kuanzia jana Aprili 28. Kwa sasa askari wa usalama Barabarani wameamua kusimama kwenye njia panda zote kwa ajili ya kutoa elimu na maelekezo kwa madereva wasioelewa mabadiliko hayo ama wasiosikia kuhusu mabadiliko hayo kabla ya kuanza kuyakamata magari yanayokiuka muongozi wa njia hizo.
 Kutokana na kwamba baadhi ya madereva bado hawajaelewa mabadiliko hayo, askari hao wamekuwa wakisimama eneo husika na kuwasimamisha wakati wakitaka kuelekea na kusha kuwapatia elimu na kisha kuwaruhu kuendelea hadi hapo watakapositisha elimu hiyo na kuanza kuwakamata madereva wasiofuata sheria na alama hizo. Hii ni barabara ya Karimjee ambayo kwa sasa haiendi ukitokea Ocean Road.
 Hii ni barabara ya Samora ambayo kwa sasa inapandisha ukitokea mzunguko wa Askari.....
Hii ni barabara ya mbele ya Maelezo na Jengo la IPS ambayo kwa sasa haielekei bali inapandisha usawa wa Mzunguko wa Askari....

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI