Tuesday, September 16, 2014

KUHUSU ASKARI WA USALAMA BARABARANI ALIYEGONGWA NA DCM MBAGALA, DAR

ASKARI wa usalama barabarani, aliyejulikana kwa jina la Riziki, WP 2806 Cpl Riziki, akiwa hoi baada ya kugongwa na daladala aina ya DCM wakati akiwa katika harakati za kutimiza majukumu ya kazi eneo la Mbagala Rangi Tatu, jana asubuhi.
Habari zinasema kuwa baada ya ajali hiyo, askari huyo alikimbizwa katika hospitali ya Temeke na baadaye kuhamishiwa hospitali ya Muhimbili na hali yake inaendelea vizuri.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI