Friday, May 30, 2014

ROSTAM AZIZI KATIKA MSIBA MKUBWA

ALIYEKUWA mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, (CCM), amefiwa na baba yake Aziz Abdulrasool (73) jijini Dar es Salaam jana asubuhi. Akizungumza nyumbani kwa marehemu Oysterbay jana, mtoto wa pili wa marehemu, Akram Aziz, alisema baba yake alifariki saa 12 asubuhi ikiwa ni saa mbili tu baada ya kurudishwa nchini kutoka Ufaransa alikuwa anatibiwa. “Baba amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa saratani,tumemrudisha nchini jana saa 10 alfajiri kutoka Ufaransa, lakini ilipofika saa 12:30 alifariki dunia. 

“Baada ya kugundulika kuwa na saratani, alianza matibabu Nchini Ufaransa na Kurudi hapa Nyumbani…Mara ya mwisho baba alipelekwa nje miezi miwili iliyopita, lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya akaomba tumrudishe nyumbani ili awe karibu na ndugu na mafariki zake,”alisema Akram. 
Marehemu alizikwa jana katika makaburi ya Kisutu, saa 10 jioni jijini Dar es Salaam na amewacha wajane watatu,watoto 17 na wajukuu nane.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI