Friday, September 26, 2014

BILIONEA 'JACK MA YUN ALIBABA' NDIYE TAJIRI MKUBWA NCHINI CHINA

MWAKILISHI wa mtandao wa Alibaba ndiye tajiri mkubwa zaidi nchini Uchina kulingana na rekodi za kampuni yake.
Hili imethibitishwa na ripoti rasmi ya kifedha ya Hurun.
Bw. Ma ameongoza orodha ya watu tajiri zaidi nchini Uchina kwa mali ya takriban dola bilioni 25 akifuatwa na mwenyekiti wa Wanda Group Wang Jianlin.
Matajiri watano katika ya kumi walio katika orodha hiyo, wanamiliki kampuni za mitandaoni huku wakiwabwaga wale wanaomiliki mali isiyohamishika ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiongoza orodha hiyo.
Matajiri nchini Uchina: 
JINA, KAMPUNI
Orodha hiyo inahusisha pia kiongozi wa Tencent Pony Ma.
Mabwenyenye wengine walio katika orodha hiyo ni mwanzilishi mwenza wa mtandao wa intanet marufu sana nchini China Baidu, Robin Li na pia mwanzilishi wa soko la mtandao la JD.com, Richard Liu Qiangdong.
Bw Liu ambaye kampuni yake ilihusika katika ubadilishanaji wa hisa huko New York hapo Agosti mwaka huu, aliorodheshwa katika nafasi ya kumi.
Kulingana na mtafiti mkuu ambaye pia ndiye mwenyekiti wa Hurun Report, Rupert Hoogewerf amesema orodha hiyo imeonyesha kwamba ari ya kufanya biashara kati ya wananchi wa Uchina bado haijafa.
"Jack Ma ambaye ameorodheshwa wa kwanza, ni wa kumi na moja kuwahi kushikilia nafasi hiyo katika muda wa miaka 16. Hii inaonyesha mabadiliko makubwa katika uchumi wa Uchina na kutukumbusha uwezo ulio na masoko mapya yanayojitokeza kwa sasa.”
Orodha ya matajiri inayotolewa na Hurun Report ndiyo inayoaminika sana kwa kuwa hukadiria vizuri utajiri nchini Uchina

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI