Friday, September 26, 2014

HABARI NZURI KWA AFRIKA: CHANJO YA EBOLA KUPATIKANA HIVI KARIBUNI

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa, chanjo ya ugonjwa wa Ebola inaweza kuwa tayari kwa kiasi kikubwa mwishoni mwa mwaka huu ili kusaidia kupambana na virusi vya ugonjwa huo katika nchi za magharibi mwa Afrika.
WHO aidha imesema, kiasi cha chanjo hiyo kitakuwa cha kutosha kuweza kusaidia kudhibiti ugonjwa wa Ebola kwenye eneo hilo. 
Tangazo hilo limetolewa kufuatia uchunguzi uliofanywa na taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa ulioonesha kuwa asilimia 70 ya watu walioambukizwa virusi vya ugonjwa huo huko magharibi mwa Afrika wamefariki dunia.
Itakumbukwa kuwa, kuanzia tarehe 19 Septemba mwaka huu, idadi ya walioambukizwa ugonjwa huo katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone imeongezeka mno na kufikia watu 5,843, huku watu wapatao 2,800 wakiwa wamefariki dunia kutokana na ugonjwa huo.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI