Friday, October 17, 2014

DIAMOND KUWEKA JINA LAKE BADALA YA NAMBA ZA USAJILI KATIKA GARI YAKE MPYA ALIYOZAWADIWA

 
NI wiki zinahesabika toka staa wa bongofleva Nay wa Mitego apate namba mpya ya gari lake inayoendana na ile ambayo amekua akiitaja kwenye nyimbo zake na kwenye page zake za mitandao ya kijamii. #966 
Stori nyingine ya leo ni kutoka kwa staa mwingine wa bongofleva ambae kila anaefatilia huu muziki hapa bongo anamfahamu, ni yuleyule ambae amevunja rekodi ya kuwa staa pekee wa Tanzania alieandikwa sana kwenye mitandao ya kijamii na magazetini kwa miaka miwili mfululizo. 
Ni Diamond Platnumz ambae kwenye birthday yake hivi karibuni management yake ilimzawadia gari aina ya BMW X 5 ambapo inaaminika amechukua namba hizi kwa ajili ya mkoko wake aliozawadiwa……….. atakua msanii wa kwanza kuweka jina lake badala ya namba kwenye gari. 
Utaratibu wa kuweka majina badala ya namba umeanza kutumika kihalali nchini Tanzania ambapo watu mbalimbali wasio maarufu walishaanza kujiwekea miezi kadhaa iliyopita ambapo ada yake ni milioni tano kwa miaka mitatu.
 
Mpango wa mastaa kuweka majina kwenye magari yao badala ya namba tulizozizoea umekua ukitumika kwenye nchi mbalimbali duniani ambapo kwa Afrika Mashariki Uganda ndio inaongoza kwa kuwa na mastaa wengi waliotundika majina kwenye mikoko yao. 

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI