Saturday, May 17, 2014

INAYOMHUSU MWANAMKE ALIYEHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUASI DINI SUDAN

Serikali imesema kuwa Sudan 
sio nchi ya kwanza kutekeleza 
sheria za kiisilamu
MAHAKAMA nchini Sudan imemhukumu 
kifo mwanamke mmoja anayedaiwa kubadili dini 
yake na kuolewa na mwanamume mkristo.
Daktari Mariam Yahya Ibrahim Ishag, ambaye babake 
ni muisilamu alishitakiwa kwa kosa la kuasi dini 
pamoja na kufanya zinaa kwa kuolewa na 
mwanamume mkristo , kitu ambacho dini ya 
kiisilamu imeharamisha kwa wanawake.

Sudan!

Mariam mwenye umri wa miaka 28 pia ni mjamzito 
na ataadhabiwa kwa kuchapwa mijeledi miamoja 
kwa kosa la zinaa.

Maafisa wakuu wanasema kuwa licha ya 
Mariam kulelewa kwa njia ya kikristo yeye bado 
ni muisilamu kwa sababu hiyo ndiyo dini ya babake.
Alipewa siku tatu baada ya kuhukumiwa aweze 
kurejea katika dini ya kiisilamu lakini akakataa na 
ndio maana adhabu ikasalia.
Kwa kawaida wanawake waisilamu 
hawaruhusiwi kuolewa na wanaume wakristo 
ingawa wanaume waisilamu wanaruhusiwa 
kuwaoa wanawake wakristo.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za 
binadamu Amnesty International linasema kuwa 
Bi Ishag alilelewa kama Mkristo muorthodoxi 
kwa sababu babake hakuwepo naye maishani mwake.
'Kesi ya kwanza'

Kesi ya Ibrahim ni ya kwanza ya aina yake 
kusikika nchini Sudan , kwa mujibu wa shirika la 
habari la Reuters.

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu, 
wamelaani uamuzi huo wa mahakama na 
kuitaka serikali ya Sudan kuheshimu haki na uhuru 
wa watu kuabudu.


Maafisa wa balozi za mataifa ya magharibi 
pia wamekemea vikali kesi hiyo na kuelezea asiwasi 
wao kuihusu.
Maafisa hao wamewataka maafisa wa sheria 
nchini humo kuangalia kesi hiyo upya na 
kuhakikisha kuwa Mariam anatendewa haki.
Waziri wa mawasiliano amesema kuwa sio Sudan 
peke yake ambako sheria za kiisilamu zinafuatwa 
na ambako sio sawa kwa mtu kubadili dini yake, 
hali hiyo pia ipo nchini Saudi Arabia na katika 
nchi zingine zinazofuata sheria za kiisilamu.
Serikali ya Rais Omar al-Bashir inakabiliwa 
na changamoto nyingi za kiuchumi na kisiasa hasa 
baada ya kujitenga na Sudan Kusini ambako 
mafuta yake yalikuwa yanatoka mwaka 2011

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI