Saturday, June 7, 2014

MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO WAASWA KUTOA TAARIFA ZINAZOHUSU TAASISI ZAO KWA WAKATI

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel  akifurahia jambo na Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Innocent Mungy, Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Sylvia Lupembe na Katibu Mwenezi wa Chama hicho Bw. Abel Ngapemba.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akiongea na Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali wakati wa Semina ya Mafunzo iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel na Kulia ni Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Innocent Mungy.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel wakati wa Semina ya Mafunzo iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Leo Jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Sylvia Lupembe akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga, wakati wa Semina ya Mafunzo iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel  akiwasilisha mada kuhusu huduma kwa mteja kwa Maafisa Habari na Mawasiliano wakati wa Semina ya Mafunzo iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Leo Jijini Dar es Salaam.


0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI