Saturday, June 14, 2014

HEE YAMEKUWA HAYA TENA!!? ALICHOSEMA LULU JUU YA UHUSIANO WA KIMAPENZI NA NANDO

MTOTO mzuri Bongo Movies, Elizabeth 
Michael 'Lulu' ameibuka na kufunguka kuwa 
amekerwa na kitendo cha mshiriki wa 
Shindano la Big Brother Africa (BBA) 2013, 
Amir Khan Nando kujinadi kuwa aliwahi 
kuwa 'mtu' wake kitu ambacho si cha kweli. 
Akizungumza juzikati, Lulu alikiri kuwa 
Nando aliwahi kumtokea na alimkubalia 
awe 'my baby' wake lakini baada ya 
kumshtukia kuwa hana nia nzuri, 
alimpotezea kabla hawajazama kwenye 
dimbwi la mahaba. 
"Nahisi Nando alikuwa kwanza anataka kiki 
kupitia mimi na ndiyo maana kila alipotaka 
kupiga picha na mimi, nilimkatalia coz 
nilishamgundua nia yake, nimemshangaa 
kweli alipotangaza kuwa niliwahi kuwa 
mpenzi wake labda alivyonitokea na 
kumkubalia lakini sikufanya naye chochote 
kinachohusu mapenzi ndiyo akaona aseme 
hivyo," alisema Lulu. 
Juzikati, Nando alifanya mahojiano na 
Global TV Online ambapo awali alidai 
'kutembea' na Lulu lakini alipobanwa zaidi 
aliumauma maneno na kudai anampenda 
na yuko tayari kumuoa kwa sababu ana sifa 

za kuwa mke (wife material).

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI