Saturday, June 14, 2014

MAKUBWA HAYA!!! YAJUE YA MWANAMKE ALIBEBA MIMBA KWA MIEZI 9 NA KUJIFUNGUA MJUSI

MWANAMKE mmoja nchini Indonesia 
amejifungua mjusi badala ya mtoto. 
Mwanamke huyo Debi Nubatonis, mwenye 
umri wa miaka 31, ameanza kupata vitisho 
kutoka kwa kundi la vijana kutokana na 
kitendo hicho wakimtuhumu kwa uchawi 
ambapo sasa mamlaka za nchi hiyo 
zimetuma timu ya wataalamu kwa ajili ya 
kumaliza utata wa tukio hilo lisilo la 
kawaida. 
Wanasayansi katika timu inayofanya 
uchunguzi kwa mwanamke huyo 
wamesema wanahitaji kupatiwa muda wa 
kutosha kuchunguza tukio hilo na kuja na 
maelezo ya kueleweka. 
Kitendo hicho cha mwanamke kujifungua 
mjusi badala ya mtoto kilibainishwa na 
mkunga anayedai kwenda nyumbani kwa 
mwanamama huyo kumsaidia kujifungua 
katika kijiji cha Oenunto kwakuwa 
alishindwa kufika hospitalini. 
Madai ya mwanamke huyo kujifungua mjusi 
yameibua vitisho dhidi ya mwanamke huyo 
na familia yake ambao wanatuhumiwa kwa 
uchawi na kuamsha mjadala mkubwa 

katika mitandao

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI