Tuesday, November 15, 2016

MATANGAZO YAZIDI KUMPAISHA DAVID BECKHAM

MWANASOKA wa zamani wa Uingereza David Beckham bado anaendelea kuingiza pesa nyingi licha ya kuwa amestaafu soka amepata zaidi ya Pound milioni 11, kupitia dili za matangazo tu anazofanya kupitia jina na muonekano wake.
David Beckham amekuwa akitengeneza pesa nyingi kupitia kampuni yake ya Footwork Productions na bidha kama whisky na vifaa vya michezo ndio vimempa pesa nyingi zaidi.
Mwaka 2016 Mwezi wa tatu David Beckham alitajwa kuwa namba mbili kwenye orodha ya wanamichezo waliostaafu wanaoingiza pesa nyingi zaidi, namba moja ikishikiliwa na mcheza kikapu maarufu Michael Jordan, akiwa ametengeneza Pound milioni 69 mwaka 2015.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI