Thursday, November 13, 2014

NAY WA MITEGO AFUNGUKA - 'NAJIVUNIA KUZAA NA SIWEMA'

MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefunguka kuwa japokuwa ana watoto wengine wa nje lakini anajivunia kuzaa na mkewe, Siwema kwani walipitia changamoto nyingi kabla ya kupata mtoto.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa na mpenzi wake Siwema.
Akichezesha taya na paparazi wetu, Nay alisema katika maisha ya mapenzi yake na Siwema walivumilia vingi na hivi sasa ana mshukuru Mungu kwani wameweza kufikia hatua nzuri ya kupata mtoto.
“Maisha ya mapenzi yetu yalikuwa na changamoto sana lakini nilisimama kwa sababu nampenda mke wangu Siwema, najivunia kuzaa na Siwema mtoto wa kiume na ninaendelea kumuomba Mungu aendelee kumkuza mwanetu,” alisema Nay wa Mitego.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego
Wadau mbalimbali wamekuwa wakimpongeza Nay kwenye mitandao ya kijamii kwa kile wanachodai kwamba ana mapenzi ya kweli licha ya changamoto nyingi zilizojitokeza kwa mpenzi wake Siwema za picha kuzagaa mitandaoni kwamba alikuwa mchumba wa mtu.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI