Sunday, January 4, 2015

MMMMH HII NAYO SASA BALAA: MAMA KIJACHO AUNT EZEKIEL NA MARTIN KADINDA WANASWA WAKITOMASANA! *PICHA*


MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda na mwigizaji Aunt Ezekiel wamenaswa chobingo wakiwa katika pozi tata.
Tukio hilo lililoibua maswali mengi yasiyokuwa na majibu lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika Klabu ya 71, Tegeta-Kibaoni jijini Dar kulipokuwa na shoo ya kuukaribisha mwaka iliyoandaliwa na Kampuni ya Endless Fame.
Mwanamitindo maarufu Bongo, Martin Kadinda na mwigizaji Aunt Ezekiel wakiwa kwenye pozi tata.
“Mh jamani huyu Aunt si ana mume? Halafu si ana kibuzi chake kingine? Huyu Martin naye imekuwaje tena,” alisikika jamaa mmoja ukumbini humo.
Alipoulizwa Aunt kuhusu tukio hilo, alisema wamekumbatiana kirafiki tu na si wapenzi.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI