Monday, November 3, 2014

UGONJWA WA EBOLA WAGEUZWA MTAJI: MSANII CAM'RON AINGIZA SOKONI MASK ZA EBOLA ZAIDI YA ELFU 5

RAPPER Cam'ron aliyetangaza hivi karibuni kuwa anauza mask za kuziba midomo na pua kwa wale wanaotaka kujikinga na Ebola na bado kuwa na muonekano mzuri amesema mpaka sasa ameuza mask 5000.
Akiongea na Tmz Cam'ron aliulizwa kama mask hizo zinaweza kuzuia Ebola, alichojibu ni kwamba yeye sio mwana sayansi wala mtalamu wa magonjwa ila kama upo tayari kununua mask zinazouzwa kwenye maduka ya dawa za mafua basi ata zake zinafanya kazi hiyo.

Mask ya Cam'ron inauzwa dola 19.99 na zitasambazwa kwenye maduka sehemu tofauti duniani November 7.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI