Tuesday, November 11, 2014

PALE MISS TANZANIA ALIPOAMUA KUVUA GAMBA, HAYA YALIZUNGUMZWA KWA KINA *PICHAZ*

Mrembo aliyetawazwa umalkia wa Tanzania 2014, 'Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtevu (pichani kushoto) ametangaza rasmi kujivua taji hilo. Pamoja naye ni Mkurugenzi wa Lino International Agency Hashim Lundenga, ambao ndio waandaaji wa Miss Tanzania akizungumza japo katika moja ya mikutano na waandishi ambayo ilihusiana na taji hilo la Miss Tanzania 2014 kushikiliwa na Sitti ilhali anashutumiwa kudanganya umri. 

Pasi nakuwepo mrembo huyo Lundenga, alisoma barua iliyoandikwa na mrembo huyo na kubainisha kuwa, Sitti Mtemvu ameamua kulivua taji hilo kwa hiari yake mwenye bila shinikizo ili kuepukana na maneno ya kumchafua dhidi yake na kuilinda heshima yake, ya familia ya Mtemvu na Kamati ya Miss Tanzania.

"Sasa kwa hiari yangu mwenyewe tena bila ya kushawishiwa na mtu, na kwa kulinda heshima yangu, pamoja na famnilia yangu natamka rasmi kuvua taji la Miss Tanzania 2014," ilisemema sehemu ya barua hiyo. 

Sitti katika barua yake hiyo kuwa tangu kushinda taji hilo kumezuka shutuma mbalimbali dhidi yake, wamemuwekea maneno mengi sana mdomoni kwamba ameyasema wakati siyo, shutuma hizo zimekuwa zikiandikwa katika vyombo vya habari, blogs na mitandao ya kijamii kiasi ambacho ameona kinaweza hata kuhatarisha maisha yake.

Uamuzi wa kujivua taji hilo uliandikwa katika barua iliyotumwa kwenye kamati ya mashindano ya Miss Tanzania tangu Jumatano ya wiki hii, ambapo Lundenga alisema kuwa wamekubaliana na ombi la mrembo huyo.

Kamati ya Miss Tanzania imemvika rasmi taji hilio Mrembo aliyekuwa am,eshika nafasi ya pili, Lilian Kamazima na sasa ndiye Miss Tanzania 2014.

0 comments:

Post a Comment