Saturday, October 11, 2014

MCHEZAJI WA DRAFT MWENYE UMRI MDOGO MAREKANI

Mchezaji mwenye umri mdogo nchini Marekani katika mchezo wa drafti (chess), Sammuel Sevian, huenda akatwaa ubingwa wa  juu katika mchezo  huo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 13 tayari ameonyesha kiwango cha hali ya juu katika mchezo huo na tayari ameshaweka historia ya kuwa  bingwa katika michezo ya  kimataifa iliyofanyika mwaka jana.

Malengo ya Samuel katika mchezo huo ni  kuwa bingwa na  ana ndoto ya  kuwa bingwa mwenye umri mdogo kuiwakilisha Marekani katika mchezo wa drafti.

Licha ya mafanikio hayo Samuel anasema kuwa draft ni mchezo mgumu na kwamba ni vigumu kumwelezea mtu asiyejua  kucheza.

Samuel alianza kuonyesha mapenzi na  mchezo wa draft akiwa na na umri wa miaka mitano baada ya kufundishwa na baba yake na inaelezwa kuwa  ni vigumu kumshauri kufanya jambo lingine mbali na draft.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI