Friday, September 19, 2014

ANASWA LAIVU KWA KUUNDA MTAMBO WA KUWAIBIA AZAM, ZUKU.

 
Bw. Ali anayedaiwa kuunganisha visivyo halali, mitambo ya kurusha matangazo ya televisheni ya vituo mbalimbali kwa malipo rahisi. 
Katika hali ya kushangaza, mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Ali, mkazi wa Mwananyamala jijini Dar, amekamatwa na polisi baada ya kudaiwa kuunganisha visivyo halali, mitambo ambayo iliwawezesha watu kuangalia matangazo ya televisheni ya vituo mbalimbali kwa malipo rahisi.

Awali, msamaria mwema mmoja alipiga simu kwa kikosi kazi cha Operesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers na kukitonya juu ya uwezo wa mtu huyo anayewashangaza kwa utaalamu wake wa kuunganisha mitambo hiyo bila kugundulika.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI