Sunday, September 13, 2015

TAARIFA KUHUSU WATANZANIA WALIOKO MECCA SAUDI ARABIA BAADA YA AJALI KUTOKEA MSIKITI MKUU..!!!

Moja ya Habari zilizogusa Vichwa vingi vya Habari Duniani September 12 2015 ilikuwa Breaking News ya kuanguka kwa winch ya kujengea ambayo ilikuwa inatumika kwenye ujenzi wa eneo la pembeni ya Msikiti Mtakatifu wa Mecca, uliopo Saudi Arabia ambako waumini wengi wa Dini ya Kiislamu huwa wanakwenda kwa ajili ya Hijjah.
Taarifa Rasmi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imetolewa na inahusu hali ya Watanzania ambao wako Mecca kwa ajili ya Hijjah… Taarifa hiyo inasema hakuna Mtanzania yoyote ambaye amejeruhiwa wala kuumia kutokana na ajali hiyo.
Hijjah
Idadi ya watu waliofariki ni 107 na wengine 200 wamepata majeraha… MUNGU awapumzishe kwa amani wote waliofariki na awape nafuu pia wote waliopata majeraha kwenye ajali hiyo.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI