Thursday, September 18, 2014

CHADEMA KUMSINDIKIZA MBOWE LEO KWENDA MAKAO MAKUU YA POLISI

Mwanasheria mkuu wa CHADEMA akizungumza na wanahabari muda huu
CHAMA cha democrasia na maendeleo CHADEMA leo kimetangaza kuwa mwenyekiti wao keshoi ataenda polisi makao makuu kuitikia wito wa jeshi hilo ambao ulikuja kwa barua ukimhitaji mwenyekiti huyo kufika makao makuu ya jeshi hilo.
Kauli hiyo imetangazwa muda huu makao makuu ya chama hicho na  wanasheria mkuu wa chama hicho mbunge TUNDU LISSU wakati akizungumzia wito wa jeshi la polisi kumhitaji mwenyekiti wao kwa kile ambacho ameadi kuwa hakijawekwa wazi wanamwitia nini.
"Tumepokea barua ya jeshi la polisi makao makuu wakimtaka mwenyekiti wetu kufika makao makuu ya polisi kwa maelezo, kamati kuu ya chama imeridhia mwenyekiti aende ila hawezi kwenda mwenyewe hivyo wanasheria wote wa chama walioko mkoani Dar es salaam watamsindikiza kwa ajili ya kujua mwenyekiti wetu ameitiwa nini.hivyo tunaomba wanasheria wote wa chama kesho tukutane polisi makao makuu saa tano kwa ajili ya kumsindikiza.
Naibu katibu mkuu wa chama  JOHN MNYIKA akizungumza 
Aidha naibu katibu mkuu wa chama  hicho mh JOHN MNYIKA naye amewataka wananchi na wapenzi wa chama hicho kujitokeza kumsindikiza mwenyekiti wao kwa ajili ya kusikiliza kile ambacho mwenyekiti wao ameitiwa nini na jeshi la polisi 
Chanzo: Habaari 24

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI